Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 5:44 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

44 Lakini mimi ninawaambia: muwapende waadui zenu na muwaombee wale wanaowatesa.

Gade chapit la Kopi




Matayo 5:44
21 Referans Kwoze  

Mumwombe Mungu awabariki wale wanaowatesa; muwaombee baraka wala musiwalaani.


Musirudishiane mabaya kwa mabaya au matusi kwa matusi, lakini muombeane baraka, kwa sababu Mungu aliahidi kuwabariki ninyi wakati alipowaita kumufuata.


Halafu Yesu akasema: “Baba uwasamehe, kwa maana hawajui jambo wanalofanya.” Waaskari wakagawanya nguo zake kwa kuzipigia kura.


Wakati walipomutukana, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutisha watu hata wamwogope. Lakini alijiachilia katika mikono ya Mungu anayehukumu watu kwa haki.


Kisha akapiga magoti, akalalamika, akisema: “Bwana, usiwahesabie zambi hii.” Na nyuma ya kusema maneno haya, akakufa.


Elisha akajibu: “Hapana, usiwaue. Maana hawa unaotaka kuwaua uliwateka kwa upanga wako na mushale wako? Uwape chakula na maji, wakule na kunywa kisha uwaache warudie kwa bwana wao.”


Ee Yawe, Mungu wangu! Kama nimetenda moja ya mambo haya: kama nimechafua mikono yangu kwa ubaya,


Daudi alipomaliza kusema, Saulo akasema: “Hiyo ni sauti yako mwana wangu Daudi?” Saulo akalia kwa sauti.


Mwenye akili hakasiriki upesi; kusamehe makosa ni utukufu kwake.


Ninawapa amri mupya: mupendane ninyi kwa ninyi. Kama mimi nilivyowapenda, nanyi mupendane vilevile.


Muangalie vema, hata mumoja wenu asimurudishie mwenzake ubaya kwa ubaya, lakini mutafutiane wema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.


Lakini Paulo akalalamika kwa nguvu akisema: “Usijiue, kwa maana sisi wote tuko hapa!”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite