Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 5:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 “Heri wale wanaokuwa wamasikini wa roho, maana Ufalme wa mbinguni ni kwao!

Gade chapit la Kopi




Matayo 5:3
55 Referans Kwoze  

Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kiburi cha mutu kinamuzaraulisha mwenyewe, lakini munyenyekevu wa roho atapata heshima.


Watu wa haki wakimulilia Yawe, yeye anawasikia, na kuwaokoa katika taabu zao zote.


Afazali kuwa munyenyekevu pamoja na masikini, kuliko kugawanyana vitu vya unyanganyi pamoja na wenye kiburi.


Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


kama watu wangu hao wakijinyenyekeza, wakiomba, wakinitafuta na kuacha njia zao mbaya, basi, mimi nitawasikiliza kutokea juu mbinguni, nitawasamehe zambi yao na kustawisha inchi yao.


Ee Bwana, uniwezeshe kusema, midomo yangu itangaze sifa zako.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.


Roho wa Bwana wetu Yawe yuko pamoja nami, maana Yawe amenichagua, akanituma niwahubirie wanaoteswa habari njema, niwatunze waliovunjika moyo, niwatangazie waliohamishwa kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa.


kwa sababu umetubu na kunyenyekea mbele yangu, hata umepasua nguo yako na kulia uliposikia maneno yangu juu ya pahali hapa, na juu ya wakaaji wake, na umejinyenyekeza mbele yangu, nami vilevile nimekusikia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.


Lakini Yesu akajibu: “Heri zaidi wale wanaosikia neno la Mungu na kulitii!”


Haleluia! Heri mutu anayemuheshimu Yawe, anayefurahia sana kushika amri zake.


Heri mutu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki katika njia ya wenye zambi, wala kukusanyika na wenye kuzarau;


Kwa hiyo ninatubu na kujihukumu; ninajinyenyekeza na kuikaa juu ya mavumbi na majivu.


Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.


“Roho wa Bwana yuko pamoja nami, maana amenichagua niwahubirie wamasikini Habari Njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kwamba watakombolewa nao vipofu kwamba wataona. Amenituma kuwapa wanaoteswa uhuru,


Yesu alipoona vile, akakasirika na kuwaambia wanafunzi wake: “Muwaache watoto wadogo wakuje kwangu wala musiwakataze, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa watu wanaokuwa sawasawa na wao.


“Lakini heri kwenu, kwa sababu macho yenu yanaona na masikio yenu yanasikia!


Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe, atasimama na kuwaonea huruma. Yawe ni Mungu wa haki. Heri wote wale wanaomutumainia.


Heri mutu anayesaidiwa na Mungu wa Yakobo, mutu anayemutumainia Yawe, Mungu wake,


Wakati alipokuwa katika taabu, akamwomba Yawe, Mungu wake rehema. Akajinyenyekeza sana mbele ya Mungu wa babu zake.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.


Naye hakujinyenyekeza mbele za Yawe, kama vile Manase alivyofanya, lakini yeye aliongeza kutenda makosa zaidi.


Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.


Na Yesu akamwambia: “Umeamini kwa sababu umeniona? Heri wale wanaoamini pasipo kuona!”


Heri mutumishi yule ikiwa saa bwana wake anaporudi, anamukuta akifanya kazi ile.


Yawe Mungu ni jua na ngao yetu. Anatukubali na anatupatia utukufu. Hawanyimi kitu chochote kizuri wale wanaoishi katika ukamilifu.


Mukumbuke jinsi Yawe, Mungu wenu, alivyowaongoza katika safari ndefu kupitia katika jangwa kwa muda wa miaka hiyo makumi ine, kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kusudi ajue yanayokuwa ndani ya mioyo yenu, na kama mungeshika amri zake au hapana.


na ndugu anayekuwa tajiri afurahi kwa sababu Mungu anamushusha. Maana tajiri atatoweka kama maua ya pori.


“Sasa basi, wana wangu, munisikilize: heri wale wanaofuata njia zangu.


Maombi yake na jinsi Mungu alivyomupokea, zambi zake zote na ukosefu wa uaminifu kwake, pahali alipojenga pa kutambikia na jinsi alivyotengeneza sanamu za Ashera na sanamu zingine mbele ya kujinyenyekeza, vimeandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Waonaji.


Heri wale wanaosafisha kanzu zao, kwa maana watakuwa na haki ya kukula matunda ya muti wa uzima na ya kuingia katika muji ule kwa kupitia kwenye milango.


Halafu malaika akaniambia: “Andika maneno haya: Heri wale wanaoalikwa kwa karamu ya ndoa ya Mwana-Kondoo.” Naye akasema tena: “Maneno haya ni ya kweli yanayotoka kwa Mungu.”


Halafu mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kuume: ‘Mukuje, ninyi muliobarikiwa na Baba yangu; muingie katika Ufalme muliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa dunia.


Wimbo wa safari za kidini. Heri wote wanaomwabudu Yawe, wanaoishi kufuatana na amri zake.


Heri mutu yule mimi sitakayekuwa kikwazo kwake!”


Ninawaambia wazi kwamba watu wengi watakuja toka mashariki na magaribi, nao watachangia meza pamoja na Abrahamu, Isaka, na Yakobo kwenye karamu katika Ufalme wa mbinguni.


akisema: “Mugeuke toka zambi zenu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia!”


Lakini Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Muwaache watoto wakuje kwangu, wala musiwakataze, kwa maana Ufalme wa mbinguni ni wa watu wanaokuwa sawasawa na wao.”


Nami ninawawekea ninyi ufalme kama vile Baba yangu alivyoniwekea mimi,


kusudi mupate kula na kunywa pamoja nami katika ufalme wangu. Mutaikaa vilevile juu ya viti vya kifalme, kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.”


Wewe unajidai kwamba uko tajiri mwenye mali mengi, wala haukosewi kitu. Lakini haujui kwamba wewe ni mukosefu, mwenye taabu, masikini, kipofu na mwenye kuwa uchi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite