Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 4:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Yesu akawaambia: “Munifuate, nami nitawaweka kwa kazi ya kuopoa watu.”

Gade chapit la Kopi




Matayo 4:19
17 Referans Kwoze  

Kama mutu akitaka kunitumikia, anapaswa kunifuata, na hivi mutumishi wangu atakuwa popote nitakapokuwa. Mutu akinitumikia, Baba yangu atamupa heshima.


Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kama mutu akitaka kunifuata, ajikane yeye mwenyewe, lakini ajitolee kwa kubeba musalaba wake na kunifuata.


Naye Yesu akamwambia mutu mwingine: “Unifuate.” Lakini mutu yule akamujibu: “Bwana, unipe ruhusa niende kwanza kuzika baba yangu.”


Yesu akamujibu: “Ikiwa ninataka huyu aishi mpaka nitakaporudi, jambo hili halikuangalii! Wewe, unifuate!”


Siku iliyofuata Yesu alitaka kwenda Galilaya. Alipomukuta Filipo akamwambia: “Unifuate.”


Nyuma ya mambo hayo, Yesu alipoondoka akamwona mulipishaji mumoja wa kodi anayeitwa Lawi, akiikaa katika nyumba ya kulipishia kodi. Yesu akamwambia: “Unifuate!”


Kisha alipokuwa akipita, akamwona Lawi mwana wa Alfayo, akiikaa katika nyumba ya kulipishia kodi. Yesu akamwambia: “Unifuate!” Naye Lawi akasimama na kumufuata.


Yesu akamujibu: “Ukitaka kuwa mutimilifu, kwenda uuzishe vitu unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudi, unifuate.”


Yesu alipokuwa akipita, akamwona mutu anayeitwa Matayo, akiikaa katika nyumba ya kulipishia kodi. Yesu akamwambia: “Unifuate!” Naye akasimama na kumufuata.


Lakini Yesu akamujibu: “Unifuate mimi, uwaache hao wafu wazike wafu wao.”


Basi mutakubali kwamba mimi sikuwalemea. Lakini watu wengine wanafikiri kwamba mimi ni mwerevu na nimewanasa kwa kuwadanganya.


Yesu alipokuwa akitembea pembeni ya ziwa la Galilaya, akawaona wavuvi wawili, waliokuwa wandugu wa tumbo, Simoni (aliyeitwa Petro) na ndugu yake Andrea. Walikuwa wakitupa nyavu katika ziwa.


Mara moja wakaacha nyavu zao, na kumufuata.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite