Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 4:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Yesu alipokuwa akitembea pembeni ya ziwa la Galilaya, akawaona wavuvi wawili, waliokuwa wandugu wa tumbo, Simoni (aliyeitwa Petro) na ndugu yake Andrea. Walikuwa wakitupa nyavu katika ziwa.

Gade chapit la Kopi




Matayo 4:18
23 Referans Kwoze  

Na haya ndiyo majina ya hao mitume wake kumi na wawili: kwanza Simoni (anayeitwa vilevile Petro) na ndugu yake Andrea; Yakobo na ndugu yake Yoane, ambao ni wana wa Zebedayo;


Simoni (Yesu aliyemupa jina la Petro) na ndugu yake Andrea, Yakobo na Yoane, Filipo na Bartolomayo,


Nami sasa ninakuambia: ewe Petro, wewe ni jiwe, na juu ya jiwe hili, nitajenga musingi wa kanisa langu, na hata uwezo wa lufu hautaweza kulishinda.


Yesu akaondoka kule, akapita pembeni ya ziwa la Galilaya. Kisha akapanda kwenye kilima, naye akaikaa pale.


Nyuma ya maneno hayo, Yesu akavuka ziwa la Galilaya (linaloitwa vilevile Tiberia).


Nyuma ya mambo hayo, Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kandokando ya ziwa la Tiberia. Angalia sasa namna alivyowatokea:


Mwanafunzi wake mwingine mumoja anayeitwa Andrea, ndugu ya Simoni Petro, akamwambia:


Kisha Yesu akaondoka kule katika jimbo lililokuwa karibu na Tiro, akapita Sidona na katikati ya inchi ya Miji Kumi, hata akafika kwenye ziwa la Galilaya.


Upande wa magaribi, inchi yao ilienea mpaka muto Yordani. Toka ziwa Galilaya upande wa kaskazini, ukashuka mpaka kwenye bahari ya Araba, ni kusema bahari ya Chumvi, mpaka kwenye miteremuko ya Pisiga, upande wa mashariki.


Kutoka Sefamu utaelekea kusini mpaka Ribla, upande wa mashariki wa Aini; kisha mupaka huo utakwenda chini mpaka kwenye muteremuko wa upande wa mashariki wa ziwa la Kinereti,


Sasa, nitakutuma kwa mufalme wa Misri kusudi uwatoe watu wangu, watu wale wa Israeli, kutoka katika inchi ya Misri.”


Siku moja, Musa alikuwa anachunga kundi la kondoo la baba mukwe wake Yetro, kuhani wa Midiani. Musa akapeleka kundi lile upande wa magaribi wa jangwa, akafika kwenye mulima Horebu, mulima wa Mungu.


Wavuvi watasimama kandokando ya bahari, na nafasi toka Engedi mpaka Eni-Eglaimu itakuwa ya kuanikia nyavu. Kutakuwa aina nyingi za samaki kama zinavyokuwa katika bahari ya Mediteranea.


Yesu akawaambia: “Munifuate, nami nitawaweka kwa kazi ya kuopoa watu.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite