Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 4:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Watu hao wanaokaa katika giza, mwangaza umewatokea! Hao wanaoishi katika inchi yenye giza nzito sana ya lufu, wameona mwangaza mukubwa.”

Gade chapit la Kopi




Matayo 4:16
14 Referans Kwoze  

Wewe, ee Mungu, umeongoza taifa, umezidisha furaha yake. Watu wanafurahi mbele yako wana furaha kama kwa wakati wa mavuno, kama vile wanaogawanya vitu walivyonyanganya wanavyofurahi.


Usifurahie hali yangu ewe adui yangu! Nikianguka, nitasimama tena; nikiwa katika giza, Yawe ni mwangaza wangu.


Ndio utakaowaangazia mataifa, na kuleta utukufu kwa watu wako Waisraeli.”


Huyo aliyezifanya nyota zinazoitwa Kilimia na Orioni, ambaye analigeuza giza nene kuwa muchana, na muchana kuwa usiku; yeye anayekusanya maji ya bahari na kuyamwanga juu ya inchi kavu, Yawe ndilo jina lake.


Hakuna weusi wala giza kubwa ambamo watenda maovu wanaweza kujificha.


Mumutukuze Yawe, Mungu wenu, mbele hajawaletea giza, mbele hamujajikwaa miguu kwenye milima inayofunikwa na giza. Ninyi mulitazamia mwangaza, lakini anaugeuza kuwa usiku anaufanya kuwa giza nzito.


inchi ya huzuni na fujo, ambako mwangaza wake ni kama giza.


Itawaliwe na giza kubwa sana, mawingu mazito yaifunike. Giza la muchana liitishe!


Hatujakuasi wewe, wala hatujaiacha njia yako.


Watu waliotembea katika giza wameona mwangaza mukubwa. Watu walioishi katika inchi ya giza kubwa, sasa mwangaza umewaangazia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite