Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 3:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Mimi ninawabatiza kwa maji kwa kuonyesha kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Lakini yule atakayekuja nyuma yangu atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto. Yeye ni mwenye uwezo kunipita, nami sistahili hata kumuvua viatu.

Gade chapit la Kopi




Matayo 3:11
29 Referans Kwoze  

Basi Yoane akawaambia wote: “Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yule atakayekuja nyuma yangu ni mwenye uwezo kunipita; nami sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto.


Bwana atawatakasa wanawake wa Sayuni toka uchafu wao na kusafisha damu iliyomwangika katika Yerusalema, kwa njia ya upepo wa hukumu na wa kuunguza.


Kwa maana Yoane alibatiza kwa maji, lakini kisha siku chache, ninyi mutabatizwa kwa Roho Mutakatifu.”


Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.


alituokoa sisi. Hakufanya vile kwa sababu ya matendo yetu ya haki, lakini alituokoa kwa sababu ya huruma yake kwa njia ya Roho Mutakatifu aliyetuwezesha kuzaliwa mara ya pili na kuwa na maisha mapya kwa kutusafisha kwa maji.


Vilevile sisi wote, Wayuda na watu wa mataifa mengine, watumwa na watu wanaokuwa huru, tumebatizwa kwa Roho mumoja kusudi tukuwe mwili mumoja na sisi wote tumekunyweshwa Roho mumoja.


Waliungama zambi zao, naye Yoane aliwabatiza katika muto Yordani.


Paulo akawaambia: “Yoane aliwabatiza wale waliogeuka toka zambi zao na kuwaambia Waisraeli kwamba wamwamini yule atakayekuja nyuma yake, naye ndiye Yesu.”


Atatangulia mbele ya kufika kwa Bwana, akiwa na roho na uwezo kama nabii Elia, kwa kuwapatanisha tena baba na watoto wao, na kuwageuza waasi wapate kuwa na hekima kama vile wenye haki. Hivi atamutayarishia Bwana watu wanaokuwa tayari kwa kumupokea.”


Huyu ndiye niliyesema juu yake kwamba mutu mumoja anakuja nyuma yangu, lakini ananipita kwa sababu alikuwa mbele sijazaliwa.


Hivi Yoane alitokea katika jangwa, akibatiza watu, akiwahubiri kwamba wageuke toka zambi zao, wabatizwe, na Mungu atawasamehe.


Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa.


Nitaimwangilia maji inchi yenye kiu, na kutiririsha muto katika inchi iliyokauka. Nitajaza roho wangu juu ya wazao wako, nitawamwangia watoto wako baraka yangu.


Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


Yoane alimushuhudia akisema kwa sauti: “Huyu ndiye niliyesema juu yake: ‘Anayekuja nyuma yangu ananipita, kwa sababu alikuwa mbele sijazaliwa.’ ”


Basi Yoane akapita katika inchi zote zinazokuwa pembeni ya muto Yordani, akihubiri. Akawaambia watu wageuke toka zambi zao, wabatizwe, na Mungu atawaondolea zambi.


Walipokuwa wakiendelea na safari, wakafika kwenye nafasi moja kwenye maji, yule mukubwa akasema: “Hapa kuna maji. Ni kitu gani kinachonizuiza nisibatizwe?” [


Kisha akasimamisha gari. Filipo na yule mukubwa wakashuka wote wawili ndani ya maji na Filipo akamubatiza.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite