Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 26:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kwa maana mutakuwa na wamasikini pamoja nanyi siku zote, lakini mimi sitakuwa pamoja nanyi siku zote.

Gade chapit la Kopi




Matayo 26:11
16 Referans Kwoze  

Wamasikini hawatakosekana katika inchi; hivyo ninawaamuru, mukuwe wenye moyo safi kwa wandugu zenu wenye mahitaji na wamasikini katika inchi yenu.


Kwa maana mutakuwa na wamasikini pamoja nanyi siku zote, na munaweza kuwasaidia wakati wowote munapotaka, lakini mimi sitakuwa pamoja nanyi siku zote.


Mutakuwa na wamasikini pamoja nanyi siku zote, lakini hamutakuwa nami siku zote.”


Nilitoka kwa Baba, nami nimekuja katika dunia. Sasa ninaacha dunia na kurudi kwa Baba.”


Sasa ninarudi kwake yule aliyenituma na hakuna mumoja wenu anayeniuliza kwamba ninaenda wapi.


Kunabaki wakati kidogo, dunia haitaniona tena, lakini ninyi mutaniona; na kwa sababu mimi ninaishi, ninyi mutaishi vilevile.


Watoto wangu, ningali pamoja nanyi kwa muda mufupi tu. Mutanitafuta, lakini sawasawa nilivyowaambia Wayuda, ninawaambia ninyi vilevile kwamba hamuwezi kufika pahali ninapokwenda.


Yeye anapaswa kubaki mbinguni mpaka zitakapotimia zile nyakati Mungu atakapotengeneza vitu vyote sawa vile alivyosema tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake watakatifu.


Mimi sitabaki tena katika dunia, lakini wao wangali katika dunia na mimi ninakuja kwako. Baba Mutakatifu, uwalinde kwa uwezo wa jina lako, lile jina ulilonipa, kusudi wakuwe mumoja kama vile sisi tunavyokuwa mumoja.


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Kwa maana pahali popote watu wawili au watatu wanapokusanyika kwa ajili ya jina langu, mimi ni pale katikati yao.”


Mutu akiwa na mali ya dunia hii naye akimwona ndugu yake katika hitaji, lakini hataki kumusikilia huruma, mutu yule anaweza kusema kwamba anamupenda Mungu?


Lakini kitu kimoja walichotuomba ni kukumbuka wamasikini wa makanisa yao, nami nimefanya vile kwa bidii.


Lakini Yesu akatambua mawazo yao na kuwaambia: “Sababu gani munamusumbua mwanamuke huyu? Amenitendea jambo zuri.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite