Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 24:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Mutasikia habari za matokeo au utetezi wa vita, lakini musiogope. Sherti mambo hayo yatukie, lakini hayaonyeshi kama mwisho umefika.

Gade chapit la Kopi




Matayo 24:6
32 Referans Kwoze  

Musiogope wakati mutakaposikia habari za vita na za mapinduzi. Sherti mambo hayo yatukie kwanza, lakini haionyeshi kwamba mwisho wa dunia unatimia palepale.”


Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Musifazaike; mumwamini Mungu, na muniamini mimi vilevile.


musifazaike upesi wala kuogopa kwamba Siku ya kurudi kwa Bwana imekwisha kutimia. Inawezekana munafahamu mambo yale kwa njia ya unabii, mahubiri na barua inayosemeka kwamba imetoka kwetu.


“Ninawaachia amani; ninawapa amani yangu. Siwapatii ninyi amani hii kama dunia inavyoitoa. Musifazaike wala musiogope.


Haogopi habari mbaya; moyo wake unasimama imara na anamutegemea Yawe.


Na hii Habari Njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia nzima kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; na halafu mwisho wa dunia utatimia.


Lakini muendelee kuvumilia, maana kwa njia ile mutaokoa uzima wenu.”


Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.


Kwa maana ninawaambia, ni lazima yatimie kwangu maneno haya yaliyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Naye alihesabiwa pamoja na watenda maovu.’ Kwa sababu yanayonielekea mimi yanafikia kwa mwisho wake.”


Lakini namna gani yangetimia Maandiko Matakatifu yanayosema kwamba mambo haya yanapaswa kuwa hivi?”


Lakini watu wa Yerusalema watauzania kuwa ni utabiri wa uongo kwa sababu ya mapatano waliyofanya. Hata hivyo unabii huu utawakumbusha uovu wao na kusababisha kukamatwa kwao.


Ee upanga wa Yawe! Utatwaa muda gani ndipo utulie? Ingia katika mufuko wako, upate kutulia na kunyamaza!


Umwambie akuwe macho, atulie na asiogope wala asivunjike moyo, kwa sababu ya hasira kali ya mufalme Resini wa Aramu, na ya mwana wa Remalia. Hao wawili ni kama tu moshi wa kuni zinazozimika.


Mufalme Herode aliposikia maneno haya, akafazaika sana pamoja na wakaaji wote wa Yerusalema.


Kisha kukatokea farasi mwengine mwekundu. Na yule aliyepanda juu yake akapewa uwezo wa kuondoa amani katika dunia, kusudi watu wauane wao kwa wao. Naye akapewa upanga mukubwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite