Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 23:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Lakini ninyi musikubali kuitwa ‘Mwalimu’, kwa maana ninyi wote ni wandugu, nanyi muko na Mwalimu mumoja tu.

Gade chapit la Kopi




Matayo 23:8
34 Referans Kwoze  

Wandugu zangu, kati yenu kusikuwe walimu wengi, kwa maana munajua vema ya kuwa sisi walimu tutahukumiwa vikali zaidi kuliko watu wengine.


Musitawale kwa kinguvu kundi lile lililowekwa chini ya uangalizi wenu, lakini mukuwe mifano kwao.


Lakini mimi nimekuombea, kusudi usipungukiwe na imani. Nawe utakaponirudilia tena, uwatie wandugu zako moyo.”


Musikubali kuitwa ‘Waongozi,’ kwa maana muko na Mwongozi Mukubwa mumoja tu, ndiye Kristo.


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Mimi ni ndugu yenu Yoane. Kwa njia ya kuungana na Yesu, ninashirikiana nanyi katika mateso, katika ufalme wake na katika kuvumilia. Mimi nilikuwa nimepelekwa katika kisanga kinachoitwa Patimo, kwa sababu nilihubiri Neno la Mungu na ukweli ulioshuhudiwa na Yesu.


Lakini akaniambia: “Angalia, usifanye vile! Kwa maana mimi ni mutumishi kama vile wewe, na wandugu zako manabii na watu wanaoshika maneno ya unabii yanayoandikwa katika kitabu hiki. Ni Mungu ndiye unayepaswa kumwabudu!”


Nikaanguka mbele yake kusudi nimwabudu, lakini akaniambia: “Angalia, usifanye vile! Kwa maana mimi ni mutumishi kama vile wewe na wandugu zako wanaoshika ukweli ulioshuhudiwa na Yesu. Ni Mungu ndiye unayepaswa kumwabudu! Maana ukweli ambao Yesu alishuhudia, ndio uwezo unaowaongoza manabii.”


anayekuwa asili ya jamaa zote zinazokuwa mbinguni na katika dunia.


Kwa maana, hatutangazi habari zetu sisi wenyewe, lakini tunatangaza kwamba Yesu Kristo ndiye Bwana, nasi tuko watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.


Hatutafuti kuwaamuru ninyi juu ya mambo yale munayopaswa kuamini, maana munasimama imara katika imani. Lakini tunataka kutumika pamoja nanyi kusudi mupate kufurahi.


Yuda alipofika, akamujongelea Yesu, na kumwambia: “Jambo, Mwalimu.” Na kisha akamubusu.


Lakini inatosha kwa mwanafunzi kufanana na mwalimu wake na mutumishi kufanana na bwana wake. Ikiwa wanamwita mukubwa wa jamaa Belzebuli, hawatakosa kuwaita watu wa jamaa yake kwa majina mabaya zaidi.


Wanapenda vilevile kusalimiwa kwa heshima kwenye nafasi za makutano, na kuitwa ‘Mwalimu.’


Halafu Yuda, aliyemutoa, akamwuliza: “Mwalimu, ni mimi?” Naye Yesu akamujibu: “Wewe umesema.”


Basi Petro akamwambia Yesu: “Mwalimu, ni vizuri kuona kwamba sisi tuko hapa. Tujenge vibanda vitatu, kimoja chako, kimoja cha Musa na kingine cha Elia.”


Yesu akamwuliza: “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akamujibu: “Mwalimu, ninataka nipate kuona.”


Petro akakumbuka mambo yaliyotokea mbele, akamwambia Yesu: “Mwalimu, angalia, ule muti wa tini ulioulaani umekauka.”


Yuda alipofika, mara moja akamujongelea Yesu na kumwambia: “Mwalimu!” Kisha akamubusu.


Yesu akageuka, akawaona wakimufuata, akawauliza: “Munatafuta nini?” Wakajibu: “Rabi (maana yake ‘Mwalimu’), unakaa wapi?”


Natanaeli akamwambia tena: “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Waisraeli.”


Alimwendea Yesu usiku na kumwambia: “Mwalimu, tunajua kama Mungu amekutuma kufundisha, kwa maana hakuna mutu anayeweza kuonyesha vitambulisho hivi unavyoonyesha isipokuwa anaongozwa na Mungu.”


Basi wakamwendea Yoane na kumwambia: “Mwalimu, unakumbuka yule mutu aliyekuwa pamoja nawe ngambo ya Yordani, yule uliyemushuhudia? Angalia sasa, yeye anabatiza, na watu wote wanamufikia!”


Wakati ule wanafunzi wa Yesu walimusihi, wakisema: “Mwalimu, kula chakula.”


Watu wale wakamukuta Yesu kule ngambo ya ziwa na kumwuliza: “Mwalimu, ulifika hapa wakati gani?”


Wanafunzi wake wakamwuliza: “Mwalimu, kwa sababu gani mutu huyu alizaliwa kipofu? Ni kwa ajili ya malipizi ya zambi yake mwenyewe au zambi ya wazazi wake?”


Wanafunzi wakamwambia: “Mwalimu, hakujapita siku nyingi tokea pale Wayuda walipotaka kukutupia mawe, na sasa unataka kwenda tena kule!”


Yesu akamwambia: “Maria!” Naye akageuka, akasema kwa kiebrania: “Raboni,” maana yake “Mwalimu.”


Kwa sababu sasa yeye si kama vile mutumwa tu, lakini amekuwa bora zaidi kuliko mutumwa: yeye ni ndugu mupendwa. Mimi ninamupenda sana, nawe utamupenda zaidi sana, kwanza kama vile mutumwa, tena kama vile ndugu katika Bwana.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite