Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 23:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Wanapenda vilevile kusalimiwa kwa heshima kwenye nafasi za makutano, na kuitwa ‘Mwalimu.’

Gade chapit la Kopi




Matayo 23:7
19 Referans Kwoze  

Yesu akageuka, akawaona wakimufuata, akawauliza: “Munatafuta nini?” Wakajibu: “Rabi (maana yake ‘Mwalimu’), unakaa wapi?”


Natanaeli akamwambia tena: “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Waisraeli.”


Yesu akamwambia: “Maria!” Naye akageuka, akasema kwa kiebrania: “Raboni,” maana yake “Mwalimu.”


Watu wale wakamukuta Yesu kule ngambo ya ziwa na kumwuliza: “Mwalimu, ulifika hapa wakati gani?”


Basi wakamwendea Yoane na kumwambia: “Mwalimu, unakumbuka yule mutu aliyekuwa pamoja nawe ngambo ya Yordani, yule uliyemushuhudia? Angalia sasa, yeye anabatiza, na watu wote wanamufikia!”


Alimwendea Yesu usiku na kumwambia: “Mwalimu, tunajua kama Mungu amekutuma kufundisha, kwa maana hakuna mutu anayeweza kuonyesha vitambulisho hivi unavyoonyesha isipokuwa anaongozwa na Mungu.”


Yesu akamwuliza: “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akamujibu: “Mwalimu, ninataka nipate kuona.”


Basi Petro akamwambia Yesu: “Mwalimu, ni vizuri kuona kwamba sisi tuko hapa. Tujenge vibanda vitatu, kimoja chako, kimoja cha Musa na kingine cha Elia.”


Lakini ninyi musikubali kuitwa ‘Mwalimu’, kwa maana ninyi wote ni wandugu, nanyi muko na Mwalimu mumoja tu.


“Nitawafananisha watu wa kizazi hiki na nini? Wanafanana na watoto wanaoikaa kwenye nafasi ya makutano na kuita wenzao wakisema:


Halafu Yuda, aliyemutoa, akamwuliza: “Mwalimu, ni mimi?” Naye Yesu akamujibu: “Wewe umesema.”


Yuda alipofika, akamujongelea Yesu, na kumwambia: “Jambo, Mwalimu.” Na kisha akamubusu.


Petro akakumbuka mambo yaliyotokea mbele, akamwambia Yesu: “Mwalimu, angalia, ule muti wa tini ulioulaani umekauka.”


Katika mafundisho yake aliwaambia: “Mujiepushe na walimu wa Sheria, wanaopenda kujitembeza wakivaa kanzu ndefu, na kusalimiwa kwa heshima kwenye nafasi ya makutano.


Yuda alipofika, mara moja akamujongelea Yesu na kumwambia: “Mwalimu!” Kisha akamubusu.


“Ole kwenu, ninyi Wafarisayo! Munapenda kuikaa katika viti vya mbele ndani ya nyumba ya kuabudia na kusalimiwa kwa heshima kwenye nafasi za makutano.


Wakati ule wanafunzi wa Yesu walimusihi, wakisema: “Mwalimu, kula chakula.”


Wanafunzi wake wakamwuliza: “Mwalimu, kwa sababu gani mutu huyu alizaliwa kipofu? Ni kwa ajili ya malipizi ya zambi yake mwenyewe au zambi ya wazazi wake?”


Wanafunzi wakamwambia: “Mwalimu, hakujapita siku nyingi tokea pale Wayuda walipotaka kukutupia mawe, na sasa unataka kwenda tena kule!”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite