Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 23:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Na yeyote anayejiinua, atashushwa, lakini anayejishusha, atainuliwa.

Gade chapit la Kopi




Matayo 23:12
15 Referans Kwoze  

Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


Lakini Mungu ametujalia neema kubwa zaidi, kwa maana Maandiko yanasema: “Mungu anapingana na wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Kiburi cha mutu kinamuzaraulisha mwenyewe, lakini munyenyekevu wa roho atapata heshima.


Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Basi kila mutu atakayekuwa munyenyekevu kama huyu mutoto mudogo, ndiye atakayekuwa mukubwa katika Ufalme wa mbinguni.


Kumwogopa Yawe ni mafundisho ya hekima; mbele ya kuheshimika inafaa kuwa munyenyekevu.


“Heri wale wanaokuwa wamasikini wa roho, maana Ufalme wa mbinguni ni kwao!


Maana, Mungu anawashusha wenye majivuno, lakini anawaokoa wanyenyekevu.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Ee Yawe, ingawa wewe uko juu ya wote, unawaangalia wanyenyekevu kwa wema; lakini, unatambua wenye kiburi kwa mbali.


Basi mujinyenyekeze mbele ya Mungu mwenye uwezo, kusudi awainue kwa wakati unaofaa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite