Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 22:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Akamwuliza: ‘Rafiki, namna gani umeingia hapa bila kuvaa nguo ya karamu?’ Lakini yule mutu hakumujibu neno.

Gade chapit la Kopi




Matayo 22:12
13 Referans Kwoze  

Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


Lakini mwenye shamba akamujibu mumoja wao: ‘Rafiki, sikupunji kitu. Hatukupatana kwamba nitakulipa kikoroti kimoja cha feza kwa siku?


Hivyo wamasikini wanapata tumaini, nao uovu unakomeshwa.


Anayalinda maisha ya waaminifu wake, lakini anaangamiza maisha ya waovu katika giza. Maana, mwanadamu hapati ushindi kwa nguvu zake.


Kwa maana unajua kwamba mutu kama huyo amepotoka, na zambi zake zinamuhukumu yeye mwenyewe.


Lakini Yesu akamwambia: “Rafiki, ufanye lililokuleta.” Halafu watu wale wakajongea na kumukamata Yesu na kumufunga.


Kama vile mwizi anavyofezeheka anaponaswa, ndivyo Waisraeli watakavyofezeheka; wao wenyewe, wafalme wao, wakubwa wao, makuhani wao na manabii wao.


Namna gani basi unaweza kusema: Mimi sikujichafua wala sikufuata miungu Bali. Ukumbuke vile ulivyotenda zambi kule katika bonde; utambue yale uliyofanya huko! Wewe ni kama mwana wa ngamia, anayetangatanga huko na huko;


Watu wa usawa wanapoona jambo hilo wanafurahi, lakini waovu wote wananyamazishwa.


Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.


Basi ninawaambia: musipokuwa wenye haki kuliko walimu wa Sheria na Wafarisayo hamutapokelewa katika Ufalme wa mbinguni.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite