Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 21:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kundi la watu wakajibu: “Huyu ni nabii Yesu wa Nazareti katika Galilaya.”

Gade chapit la Kopi




Matayo 21:11
20 Referans Kwoze  

Watu walipoona kile kitambulisho Yesu alichoonyesha, wakasema: “Hakika mutu huyu ndiye yule nabii aliyepaswa kuja katika dunia!”


Watu wamoja katika kundi lile waliposikia maneno hayo, wakasema: “Hakika mutu huyu ndiye Nabii aliyepaswa kuja!”


Watu wote wakashikwa na woga, nao wakamutukuza Mungu, wakisema: “Nabii mukubwa ametokea tena kwetu! Mungu amekuja kuwasaidia watu wake.”


Ni yule yule Musa ndiye aliyewaambia watu wa Israeli: ‘Mungu atawatumia ninyi nabii anayekuwa sawa mimi, toka katika taifa lenu.’


Wafarisayo wakamwuliza tena yule aliyekuwa kipofu: “Na wewe unasema nini juu ya yule aliyekuponyesha macho?” Akajibu: “Yeye ni nabii.”


Kule akakaa katika muji ulioitwa Nazareti, kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya manabii: “Ataitwa mutu wa Nazareti.”


Halafu mwanamuke yule akamwambia: “Bwana, ninaona kama wewe ni nabii.


Halafu wakamwuliza: “Basi wewe ni nani? Wewe ni Elia?” Yoane akajibu: “Mimi si yeye.” Wakamwuliza tena: “Wewe ni yule nabii?” Naye akawajibu: “Hapana.”


Lakini wengine walisema: “Huyu ni nabii Elia.” Wengine walisema: “Yeye ni nabii sawa na mumoja wa wale manabii wa zamani.”


Naye akawauliza: “Ni mambo gani?” Nao wakamujibu: “Haujui mambo yaliyomupata Yesu wa Nazareti? Yeye alishuhudiwa na Mungu na watu wote kwamba alikuwa nabii mwenye uwezo katika mambo aliyofanya na kusema.


Wakamwuliza Yoane: “Ikiwa wewe si Kristo, wala Elia, wala yule nabii, basi sababu gani unabatiza?”


Lakini ninapaswa kuendelea na safari yangu leo, kesho na kesho kutwa, kwa sababu haipaswi nabii auawe inje ya Yerusalema.


Yule Mufarisayo aliyemwalika Yesu alipoona vile, akajisemesha: “Kama mutu huyu angekuwa kweli nabii, angetambua mwanamuke huyu anayemugusa ni wa namna gani. Angetambua kwamba yeye ni mwenye mwenendo mubaya.”


Yesu alipoingia Yerusalema, muji wote ukavuma. Watu wakaulizana: “Huyu ni nani?”


Lakini vilevile kwa kuwa tunaogopa watu hawa, hatuwezi kusema kwamba yalitoka kwa mutu; kwa maana watu hawa wote wanasadiki kwamba Yoane alikuwa nabii.”


Kwa hiyo wakatafuta kumukamata, lakini waliogopa makundi ya watu kwa sababu wao walisadiki kwamba yeye ni nabii.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite