Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Akawakusanya wakubwa wote wa makuhani na walimu wa Sheria kwa kuwauliza wapi Kristo atakapozaliwa.

Gade chapit la Kopi




Matayo 2:4
30 Referans Kwoze  

Basi kukakuwa makelele mengi, na walimu wamoja wa Sheria waliokuwa wa chama cha Wafarisayo wakasimama na kubishana kwa nguvu, wakisema: “Hatuoni ubaya wowote juu ya mutu huyu. Labda roho au malaika wamesema naye!”


Basi wakawachochea watu, wazee, na walimu wa Sheria. Nao wakamufikia Stefano, wakamukamata na kumupeleka mbele ya Baraza Kubwa.


Yesu akaingia ndani ya hekalu. Alipokuwa akifundisha, wakubwa wa makuhani pamoja na wasimamizi wa watu wakamufikia na kumwuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka yale?”


kwa maana hakuwafundisha sawa vile walimu wao wa Sheria, lakini kama vile mutu mwenye mamlaka.


Kesho yake, wasimamizi wa Wayuda, wazee na walimu wa Sheria wakakusanyika Yerusalema.


Yuda akatwaa kundi la waaskari pamoja na walinzi waliotumwa na wakubwa wa makuhani na Wafarisayo. Akakuja nao kwenye bustani wakibeba taa, mienge na silaha.


Halafu walimu wa Sheria pamoja na Wafarisayo wakaleta mbele yake mwanamuke mumoja aliyekamatwa katika uzinzi. Wakamusimamisha mbele ya watu wote


Wafarisayo wakasikia maneno hayo watu waliyosemasema juu ya Yesu. Basi wakubwa wa makuhani na Wafarisayo wakatuma walinzi wao kumufunga.


Yesu akamujibu: “Wewe unayekuwa mwalimu mukubwa katika inchi ya Israeli, haujui maneno haya?


Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria waliokuwa pale wakatoa mashitaki makubwa sana juu ya Yesu.


Saa ile ile wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria wakatafuta kumukamata, kwa sababu walitambua kwamba alisema mufano huo juu yao.


Ninyi munajidai kwamba muko na hekima, nanyi munafuata amri zangu mimi Yawe. Lakini kalamu ya uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.


Kisha Yesu akaanza kuwafundisha wanafunzi wake, akisema: “Sherti Mwana wa Mutu ateswe na kukataliwa na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani pamoja na walimu wa Sheria. Atauawa na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake atafufuka.”


Kulipokucha, wakubwa wote wa makuhani na wasimamizi wa watu wakakata shauri la kumwua Yesu.


Yesu alipokuwa hajamaliza kusema, Yuda, mumoja wa wanafunzi kumi na wawili, akafika pamoja na kundi kubwa la watu wenye panga na magongo. Hawa wote walikuwa wametumwa na wakubwa wa makuhani na wasimamizi wa watu.


Wakubwa wa makuhani na wasimamizi wa watu wakakusanyika ndani ya nyumba ya Kuhani Mukubwa, aliyeitwa Kayafa,


Lakini wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria wakachukizwa kwa kuona miujiza aliyoifanya na watoto waliokuwa wakilalamika katika hekalu, wakisema: “Usifiwe wewe, mwana wa Daudi!”


Kisha akawaambia: “Basi, kila mwalimu wa Sheria aliyefundishwa katika Ufalme wa mbinguni, anafanana na mwenye nyumba anayetwaa vitu vipya na vitu vya zamani pamoja toka katika akiba yake.”


Ni kazi ya makuhani kuwafundisha watu maarifa ya kweli juu ya Mungu kusudi watu wawaendee kwa kujifunza mapenzi yangu kwao, maana makuhani ni wajumbe wa Yawe wa majeshi.


Wafalme wa dunia wanajitayarisha, watawala wanashauriana pamoja kumwasi Yawe na muchaguliwa wake.


Ezra akasimama na kuanza kuwaapiza makuhani, viongozi, Walawi na Waisraeli wengine wote kwamba watafanya kama ilivyosemwa, nao wakakubali kufanya kiapo.


Ezra akaondoka Babeli, yeye alikuwa mwandishi mwenye ujuzi mwingi sana katika Sheria ambayo Yawe, Mungu wa Israeli, alikuwa amemupatia Musa. Na kwa musaada wa Yawe, Mungu wake, mufalme alimupatia Ezra kila kitu alichohitaji.


Hata makuhani, viongozi wa inchi ya Yuda pamoja na watu walikosa uaminifu kabisa wakiiga matendo yote ya kuchukiza ya watu wa mataifa mengine; waliichafua nyumba ya Yawe ambayo yeye mwenyewe alikuwa ameitakasa kule Yerusalema.


Kisha Hilkia akamwambia Safani mwandishi: “Nimepata kitabu cha Sheria katika nyumba ya Yawe.” Halafu Hilkia akamupatia Safani kitabu kile.


waliwasimamia wabebaji wa mizigo na kuwaongoza wote waliofanya kazi mbalimbali, na kati ya Walawi kulikuwa waandishi, wakubwa na hata walinzi wa mulango.


Mufalme Herode aliposikia maneno haya, akafazaika sana pamoja na wakaaji wote wa Yerusalema.


Nao wakamujibu: “Betelehemu katika Yudea, kwa maana ilisemwa hivi kwa njia ya nabii:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite