Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 2:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Akakaa kule mpaka Herode alipokwisha kufa, kusudi yatimie maneno haya Bwana aliyosema kwa njia ya nabii: “Nilimwita mwana wangu arudie toka Misri.”

Gade chapit la Kopi




Matayo 2:15
21 Referans Kwoze  

Israeli alipokuwa mutoto, nilimupenda. Kutoka Misri nilimwita mwana wangu.


Nawe utamwambia mufalme wa Misri kwamba Yawe anasema hivi: ‘Israeli ni mwana wangu, muzaliwa wangu wa kwanza.


Mungu aliwaondoa kutoka Misri, naye anawapigania kwa nguvu kama mbogo. Atayateketeza mataifa yanayokuwa waadui zao, atavunjavunja mifupa yao, atawachoma kwa mishale yake.


Kisha akawaambia: “Haya ndiyo maneno niliyowaambia wakati nilipokuwa ningali pamoja nanyi, kwamba sherti yatimizwe maneno yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Musa, katika maandiko ya manabii na katika Zaburi.”


Mambo hayo yote yalitukia kusudi yatimie maneno Bwana aliyosema kwa njia ya nabii:


Lakini namna gani yangetimia Maandiko Matakatifu yanayosema kwamba mambo haya yanapaswa kuwa hivi?”


Mambo hayo yote yalitokea, kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii:


Alifanya hivi kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii Isaya: “Yeye alitwaa uzaifu wetu, naye amebeba muzigo wa magonjwa yetu.”


Kule akakaa katika muji ulioitwa Nazareti, kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya manabii: “Ataitwa mutu wa Nazareti.”


Herode alipokuwa amekwisha kufa, malaika wa Bwana akamutokea Yosefu katika ndoto kule Misri.


Halafu yakatimia maneno haya yaliyosemwa kwa njia ya nabii Yeremia:


Mambo haya yalifanyika kusudi Maandiko Matakatifu yanayosema hivi yatimie: “Hakuna hata mufupa wake mumoja utakaovunjwa.”


Kisha, Yesu akiwa anajua kwamba mambo yote yametimia, akasema hivi kusudi Maandiko Matakatifu yatimie: “Ninasikia kiu.”


Mambo haya yote yamefanyika kusudi maneno yanayosemwa na manabii katika Maandiko Matakatifu yapate kutimia.” Basi wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.


“Wandugu zangu, ilikuwa lazima yale Maandiko Matakatifu yatimie ambayo Roho Mutakatifu alitabiri kwa kinywa cha mufalme Daudi juu ya Yuda, yule aliyewaongoza wale waliomukamata Yesu.


Nao walipokwisha kumutundika juu ya musalaba, wakagawanya nguo zake kwa kuzipigia kura.


Basi Yosefu akaamuka, akamutwaa mutoto pamoja na mama yake, nao wakaondoka usiku ule kwenda Misri.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite