Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 18:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 na kusema: “Kweli ninawaambia: kama musipogeuka na kuwa sawasawa na mutoto mudogo, hamutaingia katika Ufalme wa mbinguni hata kidogo.

Gade chapit la Kopi




Matayo 18:3
28 Referans Kwoze  

Kama vile watoto wachanga wanaotamani maziwa, na ninyi vilevile mukuwe na hamu ya kunywa maziwa safi ya kiroho, kusudi mupate kukomaa na kuokolewa.


Lakini Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Muwaache watoto wakuje kwangu, wala musiwakataze, kwa maana Ufalme wa mbinguni ni wa watu wanaokuwa sawasawa na wao.”


Wandugu zangu, musikuwe kama watoto kwa kufikiri: lakini katika mambo mabaya, iwatokee kutenda kama watoto wachanga. Inafaa mafikiri yenu yakuwe kama ya watu wazima.


Lakini nafsi yangu imetulia na kuwa na amani, kama mutoto muchanga anavyotulia na mama yake; ndivyo nafsi yangu inavyokuwa na utulivu.


Yesu akajibu: “Kweli, kweli ninakuambia: mutu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu.


Yesu akamujibu: “Kweli, kweli ninakuambia: mutu hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu asipozaliwa mara ya pili.”


“Mufanye nguvu muingie kwa kupitia mulango unaokuwa mwembamba; maana ninawaambia ninyi hakika: watu wengi watajaribu kuingia lakini hawataweza.


Basi mugeuke toka katika zambi, mumurudilie Mungu, kusudi awasamehe zambi zenu.


Maana mioyo ya watu hawa imegeuka kuwa migumu, wameziba masikio yao na wamefunga macho yao. Isingekuwa hivi, wangeona na macho yao, wangesikia na masikio yao, wangefahamu na mioyo yao, na wangegeukia kwangu na ningewaponyesha.


Yesu akaongeza kumwambia: “Kweli, kweli, ninawaambia: mutaona mbingu zimefunguka na wamalaika wa Mungu wakipanda na kushuka mpaka kwenye Mwana wa Mutu!”


Basi ninawaambia: musipokuwa wenye haki kuliko walimu wa Sheria na Wafarisayo hamutapokelewa katika Ufalme wa mbinguni.


Lakini mimi nimekuombea, kusudi usipungukiwe na imani. Nawe utakaponirudilia tena, uwatie wandugu zako moyo.”


kusudi ‘Wapate kuangalia, lakini wasione; nao wapate kusikia, lakini wasikuwe na ufahamu, kusudi wasipate kumugeukia Mungu na kusamehewa.’ ”


Maana kwa kufanya vile, mutaruhusiwa kabisa kuingia katika Ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.


Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”


Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kweli ninawaambia: ni vigumu sana kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni.


Maana mioyo ya watu hawa imegeuka migumu, wameziba masikio yao, nao wamefunga macho yao, kusudi wasipate kuona, nao wasipate kusikia, wala wasipate kunigeukia, nami ningewaponyesha.’


“Munapofunga kula chakula, musifanye kama wanafiki, wanaojigeuza kuwa wenye sikitiko na kukunja nyuso zao, kusudi watu waone kwamba wanafunga. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


“Munapoomba, musikuwe kama wanafiki, kwa maana wanapenda kuomba wakisimama katika nyumba za kuabudia na pembeni ya barabara, kusudi wapate kujionyesha mbele ya watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


Kisha akaniambia: Ufanye akili za watu hawa kuwa ngumu, masikio yao yasisikie, macho yao yasione; wasipate kuona kwa macho yao, wasipate kusikia kwa masikio yao, wasipate kuelewa kwa akili zao, na kunigeukia, nao wapate kupona.


“Basi wakati unapomusaidia masikini, usipige baragumu, kama vile wanafiki wanavyofanya katika nyumba za kuabudia na katika barabara kusudi wasifiwe na watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


Kweli ninawaambia: kwa muda wote mbingu na dunia vitakapokuwa vingali, hakuna hata herufi moja wala nukta moja ya Sheria itakayoondoshwa mpaka yote yatimie.


Halafu akamwita mutoto mudogo, akamusimamisha katikati yao


Basi kila mutu atakayekuwa munyenyekevu kama huyu mutoto mudogo, ndiye atakayekuwa mukubwa katika Ufalme wa mbinguni.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite