Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 18:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 “Mufanye angalisho, musimuzarau mumoja wa hawa wadogo; kwa sababu ninawaambia kwamba wamalaika wao wanaokuwa mbinguni wako siku zote karibu na Baba yangu anayekuwa mbinguni. [

Gade chapit la Kopi




Matayo 18:10
45 Referans Kwoze  

Maana Mungu atawaamuru wamalaika wake, wakulinde popote unapoenda.


Malaika ni nini, basi? Wao wote ni roho wanaomutumikia Mungu na wanaotumwa naye kwa ajili ya faida ya wale wanaopaswa kuokolewa.


Masikini alimulilia Yawe, naye akamusikia, na kumwokoa katika taabu zake zote.


Siku moja yule masikini akakufa, na wamalaika wakamupeleka mpaka pembeni ya Abrahamu. Na yule tajiri akakufa vilevile na kuzikwa.


Baragumu kubwa itapigwa, halafu atawatuma wamalaika wake katika pande ine za dunia, kusudi wawakusanye watu wake aliowachagua, kutoka katika dunia nzima.


Malaika akamujibu: “Mimi ni Gabrieli, anayebaki karibu na Mungu! Nimetumwa kusema nawe, kwa kukuletea habari hii njema.


Ni hivi vilevile Baba yenu anayekuwa mbinguni hataki hata mumoja wa hawa wadogo kupotea.


“Lakini anayeangusha mumoja wa hawa wadogo wanaoniamini, ingalikuwa heri afungiwe jiwe kubwa la kusagia katika shingo na kuzamishwa ndani ya bahari.


Herode alipokuwa amekwisha kufa, malaika wa Bwana akamutokea Yosefu katika ndoto kule Misri.


Wale watu wenye elimu walipokwisha kwenda, malaika wa Bwana akamutokea Yosefu katika ndoto na kumwambia: “Amuka, utwae mutoto pamoja na mama yake na mukimbilie Misri. Mukae kule mpaka nitakapokuambia kwamba urudie, kwa maana Herode anamutafuta mutoto kusudi amwue.”


Naye alipokuwa angali akifikiri juu ya maneno hayo, malaika wa Bwana akamutokea katika ndoto na kumwambia hivi: “Wewe Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumwoa muchumba wako Maria, kwa maana mimba yake imetokana na uwezo wa Roho Mutakatifu.


Basi kwa hiyo, yeye anayekataa mafundisho haya hamukatai mutu, lakini anamukataa Mungu anayewapa ninyi Roho wake Mutakatifu.


Basi, ninyi hamuna nyumba munamoweza kukulia na kukunywea? Au munazarau kanisa la Mungu na munataka kuwapatisha haya wale wasiokuwa na kitu? Munataka niwaambie ninyi nini? Inafaa niwasifu? Hapana, siwezi kuwasifu hata kidogo juu ya jambo hilo!


Basi hata mutu mumoja asimuzarau. Lakini mumusaidie aendelee na safari yake katika amani; kusudi apate kurudia kwangu, maana ninamungojea yeye pamoja na wandugu waamini.


Lakini wewe, kwa sababu gani unamuhukumu ndugu yako? Au wewe kwa sababu gani unamuzarau ndugu yako? Maana sisi wote tutasimama kwa kusambishwa mbele ya tribinali ya Mungu.


Kwa maana usiku malaika wa Mungu, ninayekuwa mutu wake na ninayemwabudu, alinitokea


Na pale pale malaika wa Bwana akamwazibu Herode kwa ugonjwa kwa sababu alijitukuza kwa pahali pa Mungu. Herode akakuliwa na michango ya tumbo na kisha akakufa.


Nao wakamwambia: “Uko na wazimu!” Lakini akakaza kusema kwamba ni kweli. Basi wakasema: “Ni malaika wake.”


Siku moja, ilipokuwa saa tisa ya muchana, akaona maono. Aliona waziwazi malaika wa Mungu akiingia kwake na kumwambia: “Kornelio!”


Lakini usiku malaika wa Bwana akafungua milango ya kifungo, akawaondosha mitume mule na kuwaambia:


Lakini mimi nitauona uso wako, maana mimi ni mutu wa haki; nitakapoamuka nitajaa furaha kwa sababu unanitokea.


Kisha Mikaya akasema: “Sasa sikia neno la Yawe: Nilimwona Yawe akiikaa katika kiti chake cha kifalme, na jeshi lote la mbinguni likisimama pembeni yake, upande wake wa kuume na wa kushoto.


Usijiachilie kuzarauliwa na mutu yeyote kwa sababu ungali bado kijana. Lakini ukuwe mufano kwa waamini, katika masemi yako, katika mwenendo wako, katika upendo, katika imani na katika maisha safi.


Na kwa wale wanaokuwa zaifu katika imani, ninajifanya kama muzaifu kusudi niwapate hao wanaokuwa zaifu. Kwa wote nimejifunza kuwa mwenye hali kama yao, kusudi nipate kuokoa wamoja kati yao kwa njia mbalimbali.


Sisi tunaokuwa na nguvu katika imani tunapaswa kubeba muzigo wa uzaifu wa wale wasiokuwa na nguvu. Tusifanye tu mambo yanayotupendeza wenyewe.


Ni vema kuacha kula nyama, kunywa divai na kujizuiza kufanya chochote kinachoweza kumukwaza ndugu yako.


Kisha nikaona wamalaika saba wakisimama mbele ya Mungu, nao wakapewa baragumu saba.


Wandugu zangu, kama mutu akipatikana na kosa fulani, ninyi munaoongozwa na Roho wa Mungu mumwonye mutu yule kwa roho ya upole. Na kila mumoja wenu ajiangalie mwenyewe, kusudi asijaribiwe vilevile.


Kwa sababu wengi wanasema: “Barua za Paulo ni kali na zenye maneno mazito; lakini yeye mwenyewe anapokuwa katikati yetu ni muzaifu na namna yake ya kusema ni ya kuzarauliwa.”


Sasa mimi Paulo mwenyewe ninawaomba kwa upole na kwa wema sawa na ule wa Kristo; mimi yule ambaye wanasema juu yake kwamba ni mupole wakati ninapokuwa pamoja nanyi, lakini ni mukali wakati ninapokuwa mbali nanyi.


Yesu akaongeza kuwaambia wanafunzi wake: “Yule anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; yule asiyewapokea ninyi, hanipokei mimi, na yule asiyenipokea mimi, hamupokei yule aliyenituma.”


Hatavunja tete linalokunja, wala hatazimisha taa inayofifia, mpaka aiwezeshe haki kutawala.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


Maendeleo ya ujenzi wa hekalu yanaonekana madogo, na watu wanayazarau; lakini watamwona Zerubabeli akiendelea kulijenga hekalu, nao watafurahi. Sasa, juu ya hizo taa saba, yule malaika akaniambia: Ni macho saba ya Yawe yanayoona kila nafasi katika dunia.


Washauri wake wa kawaida walikuwa Karsena, Setari, Adimata, Tarsisi, Maresi, Marsena na Memukani – viongozi saba wa Persia na Media waliokuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.


Basi, Abusaloma aliishi Yerusalema kwa muda wa miaka miwili mizima bila kumwona mufalme Daudi.


Kwa maana Kristo hakuingia katika Pahali Patakatifu palipojengwa na watu, panapokuwa tu mufano wa Pahali Patakatifu kamili, lakini aliingia katika mbingu yenyewe, pahali anaposimama sasa mbele ya Mungu kwa kututetea.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite