1 Wakati ule wanafunzi wakamufikia Yesu, wakamwuliza: “Ni nani anayekuwa mukubwa katika Ufalme wa mbinguni?”
Musifanye jambo lolote kwa roho ya mapingano wala kwa kujivuna bure, lakini munyenyekeane kila mutu akimuhesabu mwenzake kuwa muzuri kuliko yeye mwenyewe.
Lakini anayekuwa mukubwa kati yenu sherti akuwe mutumishi wenu.
Mupendane ninyi kwa ninyi kwa kweli kama vile wandugu, nanyi muheshimiane ninyi kwa ninyi.
“Si kila mutu anayeniita ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni, lakini yule tu anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.
akisema: “Mugeuke toka zambi zenu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia!”
Halafu akamwita mutoto mudogo, akamusimamisha katikati yao