Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 15:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Yesu akamujibu: “Hata ninyi vilevile hamuwezi kuelewa?

Gade chapit la Kopi




Matayo 15:16
15 Referans Kwoze  

Hamujaelewa bado? Hamukumbuki ile mikate mitano niliyoshibisha nayo watu elfu tano, nayo ile hesabu ya vitunga mulivyojaza?


Lakini wanafunzi hawakufahamu maana ya mafundisho hayo. Wakaogopa kumwuliza neno.


Naye akawaambia: “Hata ninyi vilevile hamuwezi kuelewa? Hamufahamu kwamba kila kitu kinachoingia ndani ya mutu kutoka inje hakiwezi kumuchafua?


Lakini wao hawakufahamu maana ya maneno hayo, kwa sababu yalikuwa yamefichwa kwao, kusudi wasipate kuyatambua. Nao waliogopa kumwuliza maana yake.


Kisha Yesu akaita kundi la watu na kuwaambia: “Musikilize na kuelewa maneno nitakayowaambia.


Kweli, kwa wakati huu, ninyi mungepaswa sasa kuwa walimu, lakini mungali munahitaji kufundishwa tena mafundisho ya mwanzo ya neno la Mungu. Mumegeuka tena wenye kuhitaji kunywa maziwa, wala si chakula kigumu.


Halafu akawafungua akili kusudi wapate kufahamu Maandiko Matakatifu


Wanafunzi wake hawakufahamu maana ya maneno hayo, kwa sababu yalikuwa yamefichwa kwao, nao hawakutambua kama Yesu alisema juu ya nini.


kwa maana hawakuelewa maana ya ule muujiza wa kuzidisha mikate; kwa kuwa mioyo yao ilikuwa migumu.


Namna gani hamwelewi kwamba sisemi nanyi juu ya mikate, nilipowaambia kwamba mujiepushe na chachu ya Wafarisayo na Wasadukayo.”


Yesu akawauliza watu: “Mumeelewa maneno hayo yote?” Nao wakamujibu: “Ndiyo.”


Halafu Petro akamwambia: “Utuelezee maana ya mufano huu.”


Hamwelewi kwamba kila kitu kinachoingia ndani ya kinywa, kinapita ndani ya tumbo na kisha kinatoka na kwenda katika choo?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite