Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 15:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kitu kinachoingia ndani ya kinywa cha mutu hakiwezi kumuchafua. Lakini ni kile kinachotoka ndani ya kinywa chake ndicho kinachomuchafua.”

Gade chapit la Kopi




Matayo 15:11
26 Referans Kwoze  

Hakuna kitu kinachoingia ndani ya mutu kutoka inje kinachoweza kumuchafua. Lakini kitu kinachotoka ndani yake ndicho kinachomuchafua. [


Kwa maana kazi ya Ufalme wa Mungu si kushugulika na mambo ya kula na kunywa, lakini ni kushugulika na haki, amani na furaha vinavyotolewa na Roho Mutakatifu.


Unisaidie, ee Yawe! Watu wema wamekwisha; waaminifu wametoweka kati ya watu.


Kinywa chake kimejaa laana, udanganyifu na ukorofi; ni mwepesi kusema maneno ya kuchukiza na maovu.


Usiharibu kazi ya Mungu kwa sababu ya maneno ya chakula. Hakika vyakula vyote vinaruhusiwa kukuliwa, lakini ni vibaya kwa mutu kula chakula kinachoweza kukwaza mwingine.


Musidanganywe na mafundisho mengine ya kigeni ya kila namna. Kwa maana mioyo yetu inapaswa kutiwa nguvu kwa njia ya neema ya Mungu, wala si kwa njia ya kushika kanuni zinazoagizwa juu ya vyakula. Kanuni hizo haziwafalii kitu wale wanaozishika.


Kufuatana na vile ninaungana na Bwana Yesu, ninajua hakika kwamba hakuna kitu kinachohesabiwa kichafu katika hali yake ya asili. Lakini kama mutu akihesabu kwamba kitu fulani ni kichafu, basi kitu kile ni kichafu kwake.


Wewe umemutukana nani? Umemutusi nani? Umesubutu kumufokea nani kwa majivuno? Ni Mungu, Mutakatifu wa Israeli!


Kwa maana kwa masemi yao ya kujivuna na yasiyokuwa na maana, na kwa njia ya tamaa zao mbaya za kimwili, wanawavuta watu ambao wanaanza kuwaepuka, na wale wanaoishi katika udanganyifu.


Kila kitu ni safi kwa watu wanaokuwa safi. Lakini hakuna chochote kinachokuwa safi kwa watu wachafu na wasiomwamini Mungu, kwa maana akili na zamiri zao zimekuwa chafu.


Kisha Yesu akaita kundi la watu na kuwaambia: “Musikilize na kuelewa maneno nitakayowaambia.


Halafu wanafunzi wakamufikia na kumwuliza: “Unajua kwamba Wafarisayo walikwazwa kwa kusikia maneno hayo uliyosema?”


Wao wanafundisha kwamba ni vibaya kuoana, na wanawakataza watu kula vyakula fulani fulani. Lakini Mungu aliumba vyakula vile kusudi watu waliokwisha kumwamini na kutambua ukweli wapate kuvitumia wakisha kumushukuru.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite