Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 13:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Lakini mbegu zingine zikaanguka katika udongo muzuri na kutoa matunda: zimoja zikazaa punje mia moja, zingine makumi sita na zingine makumi tatu.

Gade chapit la Kopi




Matayo 13:8
11 Referans Kwoze  

Nao udongo muzuri walimopanda mbegu, ni mufano wa watu wanaosikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mwema na kwa uhaki. Ndio wale wanaovumulia hata wanatoa matunda mazuri.


Pahali zile mbegu zilipoanguka katika udongo muzuri ni mufano wa watu wanaosikia Neno la Mungu na kulielewa. Nao wanazaa matunda; wamoja matunda mia moja, wengine makumi sita na wengine makumi tatu.”


Kama mukizaa matunda mengi, Baba yangu atatukuzwa, na hivi mutakuwa kweli wanafunzi wangu.


Mwaka ule Isaka akapanda mbegu katika inchi ile, akavuna mara mia zaidi, maana Yawe alimubariki,


Maisha yenu yatajazwa matendo ya haki ambayo Yesu Kristo anayowajalia, kwa ajili ya utukufu na sifa ya Mungu.


Kwa maana ninajua kwamba hakuna kitu kizuri kinachokaa ndani yangu, ni kusema katika hali yangu ya kimwili. Ni hivi kwa sababu ninakuwa na utashi wa kufanya jambo jema, lakini sifikii kulifanya.


Mbegu zingine zikaanguka katikati ya miiba. Ile miiba ikaota na kuzisonga.


Lakini mbegu zingine zikaanguka katika udongo muzuri, mimea ikaota, ikakomaa na kuzaa matunda: zimoja zikazaa punje makumi tatu, zingine makumi sita na zingine punje mia moja.”


Nao udongo muzuri, walimopanda mbegu, ni mufano wa watu wanaosikia Neno la Mungu na kulipokea. Nao wanazaa matunda; wamoja matunda makumi tatu, wengine makumi sita na wengine mia moja.”


Lakini mbegu zingine zikaanguka katika udongo muzuri; nazo zikaota na kutoa matunda, kila moja punje mia.” Yesu alipokwisha kuwaambia hayo yote, akasema: “Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite