Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 13:44 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

44 “Ufalme wa mbinguni unafanana na mali iliyofichwa katika shamba moja. Mutu mumoja alipoiona, akaificha tena. Halafu kwa furaha kubwa akaenda kuuzisha vitu vyake vyote na kununua lile shamba.

Gade chapit la Kopi




Matayo 13:44
29 Referans Kwoze  

kwa maana hazina zote za hekima na elimu zimefichwa ndani yake.


Ni vile inavyokuwa, hakuna mumoja wenu atakayeweza kuwa mwanafunzi wangu kama asipoacha vyote anavyokuwa navyo.”


Kwa maana pahali akiba yako inapokuwa, ni pale roho yako inapokuwa vilevile.


Na kila mutu aliyeacha nyumba yake, kaka, dada, baba, mama, watoto au mashamba kwa ajili yangu, atapokea mara nyingi zaidi na kupewa uzima wa milele.


Kupata hekima ni bora kuliko zahabu; kupata akili ni chaguo bora kuliko feza.


Nunua ukweli, wala usiuuzishe; nunua hekima, mafundisho na akili.


Kwa hiyo ninakushauria kununua kwangu zahabu iliyosafishwa kwa moto, kusudi upate kuwa tajiri. Vilevile ununue nguo nyeupe, upate kuvaa na kufunika uchi wako unaokuletea haya. Tena ununue dawa ya kutia ndani ya macho yako, kusudi upate kuona.


Halafu Petro akamwuliza: “Angalia, sisi tumeacha vyote na kukufuata wewe! Basi na sisi tutapata nini?”


Yesu akamujibu: “Ukitaka kuwa mutimilifu, kwenda uuzishe vitu unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudi, unifuate.”


Ee ninyi wote wenye kiu mukuje kwenye maji! Mukuje, wote hata musiokuwa na feza; mununue chakula na mupate kula, mununue divai na maziwa. Bila feza, bila malipo!


Na yote yaliyoandikwa zamani katika Maandiko Matakatifu yameandikwa kwa ajili ya kutufundisha sisi, kusudi tuendelee kuchunga tumaini kwa njia ya kuvumilia na kufarijiwa sawa tunavyofundishwa katika Maandiko Matakatifu.


Yesu akawaambia mufano mwingine, akisema: “Ufalme wa mbinguni unafanana na mutu mumoja aliyepanda mbegu nzuri ya ngano katika shamba lake.


Muliwahurumia wale waliokuwa katika kifungo, nanyi mulikubali kwa furaha kunyanganywa mali zenu, kwa sababu mulijua kwamba muko na mali inayokuwa bora zaidi na yenye kudumu.


Yesu akawaambia: “Mimi ni mukate wa uzima. Anayenikubali hatasikia njaa hata kidogo, na yule anayeniamini hatasikia kiu hata kidogo.


Kwa nini mupumbafu kuwa na feza katika mukono kwa kununua hekima, wakati yeye mwenyewe hana akili?


Habari za Kristo zikae ndani yenu kwa uwingi. Mufundishane na mushauriane kwa hekima. Mumwimbie Mungu kwa moyo wenu wote na kumushukuru kwa zaburi na nyimbo za kiroho.


Anayejitenga na wenzake anajipendelea mwenyewe; anakasirika akipewa shauri lolote jema.


Hakuna mutu anayejua bei ya hekima, wala hekima haipatikani katika inchi ya wanaokuwa wazima.


Alipoona ushanga mumoja muzuri sana, akaenda kuuzisha vitu vyake vyote na kuununua.


“Ufalme wa mbinguni unafanana vilevile na wavuvi wamoja waliotupa wavu ndani ya ziwa, nao ukakusanya samaki wa kila namna.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite