Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 10:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Mutakapokuwa mukienda, muhubiri kwa watu kwamba Ufalme wa mbinguni umekaribia!

Gade chapit la Kopi




Matayo 10:7
19 Referans Kwoze  

Alihubiri habari za Ufalme wa Mungu na kuwafundisha watu juu ya Bwana Yesu Kristo bila woga na bila kuzuizwa.


akisema: “Mugeuke toka zambi zenu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia!”


Yesu akamwambia: “Uwaache hao wafu wazike wafu wao, lakini wewe uende kutangaza habari ya Ufalme wa Mungu.”


Tangia wakati huo Yesu akaanza kuhubiri, akisema: “Mugeuke toka zambi zenu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia!”


“Sheria ya Musa na maandiko ya manabii yalitangazwa mpaka kuja kwa Yoane. Tangu wakati ule, Habari Njema ya Ufalme wa Mungu inahubiriwa, na kila mutu anajiingiza kwa kinguvu ndani ya ufalme ule.


Halafu akawatuma kuhubiri habari za Ufalme wa Mungu na kuwaponyesha wagonjwa,


Roho wa Bwana wetu Yawe yuko pamoja nami, maana Yawe amenichagua, akanituma niwahubirie wanaoteswa habari njema, niwatunze waliovunjika moyo, niwatangazie waliohamishwa kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa.


Basi wanafunzi wakaondoka, wakahubiri watu kwamba wageuke toka zambi zao.


Petro alipokuwa akiingia ndani ya nyumba, Kornelio akaenda kumupokea, akapiga magoti mbele yake na kumwabudu.


Wao walichukizwa sana kwa sababu wale mitume wawili walikuwa wakiwafundisha watu na kutangaza kwao kwamba Yesu alifufuka, nao ufufuko wake unahakikisha kwamba wafu watafufuka.


Alimwendea Yesu usiku na kumwambia: “Mwalimu, tunajua kama Mungu amekutuma kufundisha, kwa maana hakuna mutu anayeweza kuonyesha vitambulisho hivi unavyoonyesha isipokuwa anaongozwa na Mungu.”


Basi wanafunzi wakaondoka, wakapita katika vijiji mbalimbali, wakihubiri Habari Njema na kuponyesha watu kila fasi.


“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [


Kwa sababu hii ninawaambia: Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa kwa watu watakaotoa matunda yanayostahili ufalme ule. [


Kati ya hawa wawili ni nani aliyefanya sawa na mapenzi ya baba yake?” Wale wakubwa wakajibu: “Ni yule wa kwanza.” Na Yesu akawaambia: “Kweli ninawaambia: Walipishaji wa kodi pamoja na makahaba wataingia mbele yenu katika Ufalme wa Mungu.


Yesu alipomaliza kutoa maagizo hayo kwa wanafunzi wake kumi na wawili, akaondoka kule, akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji ya inchi ile.


Muponyeshe wagonjwa, mufufue wafu, mutakase wenye ukoma, mufukuze pepo. Mulipokea bure, mutoe bure vilevile.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite