Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 10:41 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

41 Yule anayemupokea nabii wa Mungu, kwa sababu ni nabii, atapokea zawadi sawa nabii yule. Vilevile yule anayemupokea mwenye haki, kwa sababu ni mwenye haki, atapokea zawadi sawa yule mwenye haki.

Gade chapit la Kopi




Matayo 10:41
27 Referans Kwoze  

Kwa maana Mungu ni mwenye haki. Yeye hatasahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili yake kwa namna mulivyowasaidia watu wake na munavyoendelea kuwasaidia.


Basi, mujiangalie wenyewe, kusudi musipoteze matunda ya kazi yenu, lakini mupokee zawadi kamili.


Sasa umurudishe yule mwanamuke kwa mume wake. Abrahamu ni nabii. Atakuombea nawe utaishi. Lakini usipomurudisha, ujue kwa hakika kwamba wewe utakufa pamoja na watu wako wote.”


Ingekuwa nimechagua kazi hii kwa mapenzi yangu mwenyewe, ningeweza kungojea kupokea mushahara. Lakini kwa kuwa ni muzigo niliopewa, inanipasa kuitimiza.


Kwa maana Mwana wa Mutu atakuja na wamalaika akitukuzwa na Baba yake, halafu atamulipa kila mutu kufuatana na matendo yake.


kusudi usijionyeshe kwa watu kwamba unafunga. Jambo hilo litajulikana tu kwa Baba yako anayekuwa kwa siri. Naye Baba yako anayeona tendo unalofanya kwa siri, atakulipa.


Gayo, aliyenikaribisha na anayekaribisha kanisa zima kwa kukusanyika kwake, anawasalimia. Erasto, mulinzi wa mali ya muji, pamoja na ndugu yetu Kwarto, wanawasalimia. [


Lakini wewe, unapoomba, ingia ndani ya chumba chako, funga mulango na uombe kwa Baba yako asiyeonekana. Na Baba yako anayeona tendo unalofanya kwa siri, atakulipa.


Kisha yeye na watu wa nyumba yake wakabatizwa. Naye akatusihi akisema: “Ikiwa munakubali kweli kwamba ninamwamini Bwana, basi mufike mupange ndani ya nyumba yangu.” Akatulazimisha tuitike.


Hivi tendo lile halitatoka inje, naye Baba yako anayeona tendo unalofanya kwa siri, atakulipa.


“Mujiangalie musifanye matendo mema mbele ya watu kusudi mujionyeshe kwao. Kwa maana mukifanya hivi hamutapata faida kutoka kwa Baba yenu anayekuwa mbinguni.


Muwaambie watu wa haki jinsi wanavyokuwa na heri, maana watakula matunda ya matendo yao.


Kwa maana kila mutu anayeomba, anapewa; naye anayetafuta, anapata, naye anayepiga hodi, anafunguliwa.


Halafu nao watajibu: ‘Bwana, ni wakati gani tulipokuona ukisikia njaa, au kiu, au ukikuwa mugeni, au uchi, au mugonjwa, au mufungwa, nasi hatukukusaidia?’


Naye mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokosa kumutendea mumoja wa hawa wanaohesabiwa kuwa wadogo, hamukunitendea mimi.’


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite