Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 10:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Na haya ndiyo majina ya hao mitume wake kumi na wawili: kwanza Simoni (anayeitwa vilevile Petro) na ndugu yake Andrea; Yakobo na ndugu yake Yoane, ambao ni wana wa Zebedayo;

Gade chapit la Kopi




Matayo 10:2
44 Referans Kwoze  

Walipofika katika muji wakapanda katika chumba cha gorofi walipokuwa wanazoea kukutanana. Na waliokuwa pale ni hawa: Petro, Yoane, Yakobo, Andrea, Filipo, Toma, Bartolomayo, Matayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni wa kikundi cha Wazeloti na Yuda mwana wa Yakobo.


Yesu alipoendelea mbele kidogo, akawaona wandugu wengine wawili, Yakobo na Yoane, waliokuwa wana wa Zebedayo. Walikuwa ndani ya chombo pamoja na baba yao Zebedayo, wakitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita.


Filipo akaenda kumwambia Andrea, na kisha wote wawili wakaenda kumwelezea Yesu.


Mwanafunzi wake mwingine mumoja anayeitwa Andrea, ndugu ya Simoni Petro, akamwambia:


Yakobo na Yoane wana wa Zebedayo waliokuwa wavuvi wenzake na Simoni, walishangaa vilevile. Na Yesu akamwambia Simoni: “Usiogope; tangia sasa utafanya kazi ya kuopoa watu.”


Yesu alipokuwa akitembea pembeni ya ziwa la Galilaya, akawaona wavuvi wawili, waliokuwa wandugu wa tumbo, Simoni (aliyeitwa Petro) na ndugu yake Andrea. Walikuwa wakitupa nyavu katika ziwa.


Kwa sababu hii, Mungu anasema katika hekima yake: ‘Nitawatumia manabii na mitume; watawaua wamoja kati yao na kuwatesa wengine wao.’


Mimi ni ndugu yenu Yoane. Kwa njia ya kuungana na Yesu, ninashirikiana nanyi katika mateso, katika ufalme wake na katika kuvumilia. Mimi nilikuwa nimepelekwa katika kisanga kinachoitwa Patimo, kwa sababu nilihubiri Neno la Mungu na ukweli ulioshuhudiwa na Yesu.


Barua hii inatoka kwangu mimi muzee. Ninakuandikia wewe mama uliyechaguliwa na Mungu, pamoja na watoto wako ninaowapenda hakika. Wala si mimi peke tu ninayewapenda, lakini vilevile wale wote wanaojua ule ukweli wanawapenda ninyi,


Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.


Barua hii inatoka kwangu mimi Petro, mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi muliochaguliwa na Mungu na ambao mulisambazwa, na munaoishi kama wakimbizi kule Ponto, Galatia, Kapadokia, Azia na Bitinia.


Kwa sababu hiyo, wandugu zangu, ninyi ambao mumeitwa na Mungu na kuwa watu wake kama vile sisi, mufikiri sana juu ya Yesu, anayekuwa mutume na Kuhani Mukubwa wa imani tunayotangaza.


Ni yeye ndiye aliwapatia watu zawadi za kipekee. Amewaweka wamoja kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kuwa watangazaji wa Habari Njema, wengine kuwa wachungaji na walimu.


Kisha alimutokea Yakobo, na nyuma akawatokea mitume wote.


Akaamuru Yakobo, ndugu ya Yoane, auawe kwa upanga.


Siku moja, na saa tisa ya muchana, Petro na Yoane walienda katika hekalu kwa wakati wa maombi.


Halafu wakapiga kura, na kura ikamwangukia Matia. Naye akaongezwa katika kundi la wale mitume kumi na mumoja.


Ni huyu huyu mwanafunzi ndiye aliyeshuhudia mambo hayo na kuyaandika; nasi tunajua kwamba ushuhuda wake ni wa kweli.


Petro akageuka, akaona nyuma yao mwanafunzi yule aliyependwa na Yesu. (Ni yeye aliyeegamia kifua cha Yesu wakati wa chakula na kumwuliza: “Bwana, ni nani yule atakayekutoa?”)


Simoni Petro, Toma (anayeitwa Pacha), Natanaeli (wa muji Kana katika Galilaya), nao wana wa Zebedayo pamoja na wanafunzi wengine wawili wa Yesu, wote walikuwa pamoja.


Basi akaenda mbio kwa Simoni Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine aliyependwa na Yesu na kuwaambia: “Wameondoa maiti ya Bwana toka katika kaburi na hatujui pahali walipoiweka.”


Na kulikuwa mumoja wa wanafunzi ambaye Yesu alimupenda, na aliyekuwa akimwegamia Yesu pale kwenye chakula.


Saa ilipotimia, Yesu akaikaa kula chakula pamoja na wanafunzi wake.


Yesu akawatuma Petro na Yoane, akisema: “Mwende mututayarishie chakula cha karamu ya Pasaka.”


Mitume waliporudia toka kuhubiri wakamwelezea Yesu mambo yote waliyofanya. Kisha akaondoka pamoja nao na kwenda kwenye nafasi ya upekee karibu na muji Betesaida.


Yesu alipokuwa akiikaa kwa mulima wa Mizeituni kuelekea upande wa hekalu, Petro, Yakobo, Yoane na Andrea walipokuwa peke yao pamoja naye, wakamwuliza:


Yesu na wanafunzi wake walipotoka ndani ya ile nyumba ya kuabudia, mara moja wakaenda kwa nyumba ya Simoni na Andrea, wakiwa pamoja na Yakobo na Yoane.


Na akatwaa Petro na wana wawili wa Zebedayo na kwenda nao. Akaanza kuhuzunika na kuhangaika.


Wana wa Zebedayo pamoja na mama yao wakamufikia Yesu. Yule mama akapiga magoti mbele yake, kwa kumwomba kitu kimoja.


Nyuma ya siku sita, Yesu aliwatwaa Petro, Yakobo na ndugu yake Yoane, na kuwapeleka kwenye mulima murefu. Nao walikuwa kule peke yao.


Ni mimi Yoane niliyesikia na kuona mambo hayo. Na wakati nilipokwisha kuyasikia na kuyaona, nilianguka mbele ya malaika aliyeyaonyesha kwangu kwa kumwabudu.


Hizi ni habari za mambo yaliyofunuliwa na Yesu Kristo. Kristo alipata ufunuo huu kutoka kwa Mungu, kusudi awaonyeshe watumishi wake mambo yanayopaswa kutokea kisha kidogo. Kristo alimutuma malaika wake kwa kumujulisha mutumishi wake Yoane mambo yale.


Barua hii inatoka kwangu mimi muzee. Ninakuandikia wewe Gayo, mupendwa wangu, ninayekupenda hakika.


Enyi mbingu, nanyi watu wa Mungu pamoja na mitume na manabii wake, mufurahi kwa ajili ya mambo yaliyotokea muji ule, kwa maana Mungu amewapatia haki yenu kwa kuuhukumu!


Mitume wakarudi kwa Yesu, na kumwelezea mambo yote waliyofanya na yote waliyofundisha.


Kwa hiyo Yesu akawauliza wale wanafunzi kumi na wawili: “Nanyi munataka kwenda vilevile?”


Yesu akawajibu: “Ni mimi peke niliyewachagua ninyi kumi na wawili, lakini ingawa hivi mumoja wenu ni Shetani!”


(Alisema hivi juu ya Yuda mwana wa Simoni Iskariota, kwa maana yeye ndiye atakayemutoa, ijapokuwa alikuwa mumoja wa wale kumi na wawili.)


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite