10 Vilevile musibebe mifuko, kanzu mbili, viatu wala fimbo, kwa sababu mutumishi anastahili kupewa posho lake.
Naye akawajibu: “Mwenye kuwa na kanzu mbili atoe moja kwa yule asiyekuwa na kitu, na anayekuwa na vyakula afanye hivi vilevile.”
Saulo akamwuliza: “Lakini tukimwendea, tutamupa nini? Angalia, mikate katika mifuko yetu imekwisha na hatuna chochote cha kumupa yule mutu wa Mungu. Tuna nini?”
Wakati utakapokuja uniletee koti niliyoacha kule Troa kwa Karpo; uniletee vilevile vitabu, hasa vile vya ngozi.
Daudi akatwaa fimbo yake katika mukono, akajichagulia mawe matano mazuri kutoka kwenye kijito, akayatia katika mufuko wake wa muchungaji. Mujeledi wake ulikuwa tayari katika mukono wake, akaanza kumwendea Goliati Mufilistini.
“Mutakapoingia katika muji au katika kijiji, mutafute mutu anayekuwa tayari kwa kuwakaribisha, nanyi mukae kwake mpaka mutakapotoka kule.
Akawaagiza: “Musibebe kitu chochote kwa safari yenu isipokuwa fimbo tu. Musibebe chakula, mufuko, wala feza ndani ya mikaba yenu.
akiwaagiza: “Musibebe kitu chochote kwa safari yenu, hata ikiwa fimbo, mufuko, mukate wala feza na hata mumoja wenu asivae kanzu mbili.
Nanyi mutakula kilichotolewa mukiwa pahali popote pamoja na jamaa zenu maana ni mushahara wenu kwa sababu ya kazi yenu katika hema la mukutano.