Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 9:50 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

50 “Chumvi ni kitu kizuri. Lakini chumvi ikipoteza onjo lake, itatiwa nini kusudi ipate tena kukolea? “Muwe na chumvi ndani yenu na muishi pamoja kwa amani.”

Gade chapit la Kopi




Marko 9:50
28 Referans Kwoze  

Masemi yenu yanapaswa kuwa mazuri siku zote na yenye kufaa, munapaswa kujua kujibia kila mutu vizuri.


Kama ikiwezekana, kwa upande wenu, muishi katika amani na watu wote.


“Ninyi ni kama chumvi kwa watu wote. Lakini kama chumvi ikipoteza onjo lake, itatiwa nini ipate tena kukolea? Haifai tena hata kidogo, inabakilia kutupwa na kukanyagwa na watu.


Mujikaze kwa kuishi katika amani na watu wote na kuishi katika utakatifu, kwa sababu hakuna mutu asiyeishi katika hali hiyo atakayemwona Bwana.


Basi kwa kumaliza, wandugu zangu, kwa heri. Mujikaze kuwa wakamilifu, mufarijiane ninyi kwa ninyi, mukuwe na nia moja, muishi katika amani, na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.


Kitu cha lazima ni kwamba mukuwe na mwenendo unaolingana na mafundisho ya Habari Njema ya Kristo. Kwa hivi hata kama nikikuja kuwaona au hata kama nisipokuja, nipate tu kusikia kwamba munasimama imara katika nia moja, na kwamba wote pamoja munapigana vita kwa ajili ya imani inayotokana na Habari Njema.


Kitu kisichokuwa na onjo kinaweza kuliwa bila chumvi? Sehemu nyeupe ya yai ina utamu wowote?


Muwape heshima kubwa na kuwapenda kwa ajili ya kazi yao. Mukuwe na amani kati yenu.


Musiseme neno lolote baya, lakini kama ni lazima museme tu maneno mazuri na ambayo yanasaidia kuwajenga wengine na yanayoleta neema kwa wale wanaoyasikia.


Kwa kumaliza, ninyi wote mukuwe na mawazo na nia moja, mupendane kama wandugu waamini, mukuwe wema na wanyenyekevu.


Kwa maana mutu mwenye kasirani hawezi kutimiza mambo ya haki mbele ya Mungu.


Ujiepushe na tamaa za ujana, utafute kuishi katika haki, imani, upendo na amani pamoja na watu wote wanaomwabudu Bwana kwa moyo safi.


Ninyi ni watu wa Mungu, yeye amewapenda na kuwachagua kwa ajili yake mwenyewe. Kwa hiyo, mukuwe na moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.


Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fazili, uaminifu,


Basi, uache kusema mabaya, na kuepuka kusema uongo.


Lakini wakanyamaza, kwa sababu walikuwa wakibishana katika njia kwamba nani anayekuwa mukubwa kati yao.


Wimbo wa safari za kidini: wa Daudi. Ni jambo zuri na la kupendeza sana kwa ndugu kuishi pamoja kwa umoja.


kuwaleta mbele yangu. Makuhani watawapakaa chumvi na kuwatoa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Yawe.


“Kwa maana kila mutu atatiwa chumvi kwa moto.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite