Marko 9:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
35 Basi Yesu akaikaa, akawaita wanafunzi wake kumi na wawili na kuwaambia: “Mutu anayetaka kuwa wa kwanza anapaswa kujiweka wa mwisho kuliko wote na kuwa mutumishi wa wote.”
Lakini isikuwe hivi katikati yenu. Lakini yule anayekuwa mukubwa kati yenu sherti akuwe mudogo zaidi, na yule anayekuwa mwongozi sherti akuwe kama mutumishi.
Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”
Wewe unajitakia wewe mwenyewe mambo makubwamakubwa? Usiyatafute! Achana nayo, maana ninaleta maangamizi juu ya wanadamu wote. Pato lako ni hili: nitayaokoa maisha yako kila nafasi utakapokwenda. –Ni ujumbe wa Yawe.