Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 9:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Kila wakati yule pepo anapomukamata, anamwangusha chini, na mutoto anatoka pofu na kusaga meno, nao mwili wake unakauka. Niliomba wanafunzi wako wamufukuze yule pepo, lakini hawakuweza.”

Gade chapit la Kopi




Marko 9:18
16 Referans Kwoze  

Kweli ninawaambia: ‘Mutu anaweza kuuambia mulima huu kwamba uondoke hapa na kujitupa katika bahari.’ Na ikiwa anasema maneno yale bila shaka katika moyo wake, lakini akiamini kama jambo lile litafanyika, hakika litafanyika kwake.


Yule pepo akalalamika, akamutikisatikisa mutoto kwa nguvu na kutoka ndani yake. Mutoto akaonekana sawa amekufa, hata watu wengi wakaanza kusema kwamba amekufa.


Halafu wakamuleta mutoto kwake. Na mara moja yule pepo alipomwona Yesu, akamutikisatikisa yule mutoto kwa nguvu hata akaanguka chini, akagaagaa chini na kutoka pofu.


Nilimuleta kwa wanafunzi wako, lakini hawakuweza kumuponyesha.”


Wajumbe wa Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kumusagia Stefano meno.


Watu waovu wanaona hayo na kuuzika. Wanasaga meno kwa chuki na kutoweka. Matumaini ya mutu mubaya yanapotea bure.


Wanafanana na zoruba kubwa ya bahari na matendo yao ya haya yanaonekana kama pofu ya zoruba. Wanafanana vilevile na nyota zinazotangatanga; Mungu amekwisha kuwawekea nafasi katika giza kubwa kwa milele.


Mwanamuke mumoja Mukanana aliyeishi katika pande zile akamufikia, akilalamika, akisema: “Ee Bwana, mwana wa Daudi, unihurumie! Binti yangu anateswa sana na pepo.”


Lakini wale waliopaswa kushiriki katika Ufalme ule watatupwa inje kwenye giza, na kule watalia na kusaga meno.”


Amenirarua kwa hasira na kunichukia, amenisagia meno, na adui yangu ananitonolea macho.


Na mutu mumoja kati ya kundi akamujibu: “Mwalimu, nimemuleta mwana wangu kwako, kwa maana yuko na pepo wa bubu.


Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu! Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite