Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 8:33 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

33 Lakini Yesu akawageukia wanafunzi wake na kumukaripia Petro akisema: “Ondoka hapa karibu nami wewe Shetani, kwa maana mawazo yako si ya Mungu lakini ni ya kimutu.”

Gade chapit la Kopi




Marko 8:33
24 Referans Kwoze  

Lakini Yesu akamwambia: “Toka wewe, Shetani! Kwa maana imeandikwa: ‘Umwabudu Bwana Mungu wako na umutumikie yeye peke yake.’ ”


Musipende dunia, wala mambo yanayokuwa katika dunia. Mutu akipenda dunia, hawezi kumupenda Mungu Baba.


Mwisho wao ni uharibifu, sababu mungu wao ni kushibisha tumbo zao. Wanajivuna kwa kufanya mambo ya kuwafezehesha. Nayo mafikiri yao ni juu ya vitu vya dunia hii.


Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.


Afazali mutu mwema anipige kwa kunionya; lakini sikubali hata kidogo kusifiwa na wabaya, maana ninaomba siku zote juu ya maovu yao.


Kristo aliteswa kimwili. Basi ninyi vilevile mujikaze mupate kuwa na nia kama ile yake. Kwa maana mutu anayevumilia mateso ya mwili, anaachana kabisa na zambi.


Wale wenye kufanya zambi, uwakaripie mbele ya watu kusudi wengine wapate kuogopa vilevile.


Basi munapaswa kumutoa mutu yule kwa Shetani, kusudi mwili wake uharibiwe, nayo roho yake iweze kuokolewa Siku ile Bwana Yesu atakaporudi.


Bwana akageuka na kumwangalia Petro. Petro akakumbuka maneno yale Bwana aliyomwambia kwamba mbele jogoo hajawika atakuwa amemukana mara tatu.


Kisha akawaangalia watu waliomuzunguka, na kusema: “Mama yangu na wandugu zangu, ni hawa wanaoikaa hapa.


Yesu akawakazia macho kwa kasirani, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wao. Akamwambia yule mutu: “Nyoosha mukono wako.” Akaunyoosha, nao ukakuwa muzima tena.


Lakini Yesu hakumujibu hata neno moja. Halafu wanafunzi wake wakamufikia na kumusihi: “Umwambie aende kwa maana anatuuzi na makelele.”


Halafu Abisayi mwana wa Zeruya akasema: “Si Simei anapaswa kuuawa maana alimulaani muchaguliwa wa Yawe?”


Usimuchukie ndugu yako ndani ya moyo wako, lakini upatane siku zote na mwenzako kusudi usitende zambi.


Ushuhuda huo ni wa kweli. Basi kwa hiyo uwaonye vikali, kusudi wapate kuwa na imani kamili.


Lakini Yesu akawageukia na kuwakaripia.


Lakini Yesu akamujibu: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Umwabudu Bwana Mungu wako na umutumikie yeye peke yake.’ ”


Akamujibu: “Wewe unasema kama wanawake wapumbafu. Tukipokea mazuri kutoka kwa Mungu, kwa nini tukatae kupokea vilevile mabaya kutoka kwake?” Katika mambo hayo yote, Yobu hakusema neno lolote la kumukosea Mungu.


Lakini Yesu akageuka na kumwambia: “Ondoka hapa karibu nami, wewe Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu, kwa maana mawazo yako si ya Mungu, lakini ni ya kimutu.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite