Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 8:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Kisha Yesu akaanza kuwafundisha wanafunzi wake, akisema: “Sherti Mwana wa Mutu ateswe na kukataliwa na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani pamoja na walimu wa Sheria. Atauawa na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake atafufuka.”

Gade chapit la Kopi




Marko 8:31
27 Referans Kwoze  

“Huyu Musa ndiye yule Waisraeli waliyemukataa, wakisema: ‘Nani aliyekuweka wewe kuwa mukubwa na mwamuzi?’ Mungu alimutuma kuwa mukubwa na mukombozi wao, akisaidiwa na yule malaika aliyemutokea katikati ya kichaka kinachowaka moto.


Yesu akawajibu: “Mubomoe hekalu hili, nami nitalijenga katika siku tatu.”


Haikumupasa Kristo ateswe kama vile na aingie kwenye nafasi atakapotukuzwa?”


Lakini kwanza sherti ateswe sana na kukataliwa na watu wa kizazi hiki.


Hamujasoma bado Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Jiwe lililokataliwa na wajengaji limekuwa sasa jiwe kubwa la musingi.


Na Yesu akawaambia: “Hamujasoma bado Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Jiwe lililokataliwa na wajengaji limekuwa jiwe kubwa la musingi. Ni Bwana aliyefanya jambo hili, nalo ni ajabu sana kwetu.’


Kwa maana, kama vile Yona alivyobaki ndani ya tumbo la samaki mukubwa kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku, ndivyo vilevile Mwana wa Mutu atakavyobaki ndani ya udongo kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.


Nyuma ya siku mbili atatupatia tena uzima. Nyuma ya siku tatu atatufufua kusudi tuweze kuishi pamoja naye.


Alizikwa na kufufuliwa kwa siku ya tatu kisha kufa kwake kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema.


Kisha akawaambia: “Haya ndiyo maneno niliyowaambia wakati nilipokuwa ningali pamoja nanyi, kwamba sherti yatimizwe maneno yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Musa, katika maandiko ya manabii na katika Zaburi.”


Alizarauliwa na kukataliwa na watu. Alikuwa mutu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mutu wa kuchukiza kwa watu; alizarauliwa na tukamwona si kitu.


Jiwe lililokataliwa na wajengaji, limekuwa sasa jiwe kubwa la musingi.


Lakini leo hii mumenikataa mimi Mungu wenu ambaye ninawaokoa kutoka hasara na huzuni zenu, nanyi mumesema: ‘Hapana! Utuwekee mufalme juu yetu.’ Sasa basi, mujikusanye wote mbele yangu mukiwa katika makabila yenu na kwa maelfu yenu.”


Yawe akamwambia: “Sikiliza kila kitu ambacho watu wanakuambia; maana hawajakukataa wewe, lakini wamenikataa mimi kuwa mufalme juu yao.


Yule anayenikataa na asiyekubali maneno yangu atahukumiwa kufuatana nayo. Ni lile neno nililosema ndilo litakalomuhukumu siku ya mwisho.


na kumwambia: “Bwana, tunakumbuka kwamba wakati yule mudanganyifu alipokuwa angali muzima, alisema: ‘Kwa siku tatu kisha kufa kwangu, nitafufuka.’


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite