Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 8:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Yesu akatambua maneno waliyosema, basi akawauliza: “Sababu gani munasemezana juu ya kukosa mikate? Hamujafahamu wala kuelewa? Mioyo yenu ingali migumu?

Gade chapit la Kopi




Marko 8:17
17 Referans Kwoze  

kwa maana hawakuelewa maana ya ule muujiza wa kuzidisha mikate; kwa kuwa mioyo yao ilikuwa migumu.


Mara moja Yesu akitambua mafikiri yao, akawauliza: “Sababu gani munajiuliza mambo hayo yote?


Ee Yawe, mbona unatukosesha njia zako? Mbona unaifanya mioyo yetu kuwa migumu hata tusikuogope? Urudie, ee Mungu, kwa ajili ya watumishi wako, makabila ambayo yalikuwa mali yako siku zote.


Yesu akawakazia macho kwa kasirani, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wao. Akamwambia yule mutu: “Nyoosha mukono wako.” Akaunyoosha, nao ukakuwa muzima tena.


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


Kisha Yesu akamwuliza mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?” Basi Petro akauzika kwa sababu Yesu alimwuliza mara ya tatu kama anamupenda. Kwa hiyo akamujibu: “Bwana, unajua yote; unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia: “Tunza kondoo wangu.


Sasa tunajua kwamba unajua yote na si lazima mutu akuulize kitu. Sababu hii tunaamini kama ulitoka kwa Mungu.”


Basi Yesu akawaambia: “Enyi wajinga na wenye mioyo mizito kwa kuamini maneno yote manabii waliyosema!


Kwa mwisho Yesu akawatokea wanafunzi kumi na mumoja walipokuwa wakikula. Naye akawakaripia kwa sababu ya kutokuamini kwao na kwa sababu ya ugumu wao. Kwa maana hawakusadikia wale waliomwona nyuma ya kufufuka kwake.


Hamwelewi kwamba kila kitu kinachoingia ndani ya kinywa, kinapita ndani ya tumbo na kisha kinatoka na kwenda katika choo?


Yesu alipojua habari ile, akaondoka kule. Watu wengi wakamufuata, naye akawaponyesha wagonjwa wote.


Wanafunzi wakaanza kusemezana hivi wao kwa wao: “Anasema hivi kwa sababu hatuna mikate.”


Wanafunzi wakaanza kusemezana: “Anasema hivi kwa sababu hatuna mikate.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite