Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 7:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Kisha Yesu akaangalia juu mbinguni, akasisimua na kumwambia yule mutu: “Efata,” maana yake, “Funguka!”

Gade chapit la Kopi




Marko 7:34
21 Referans Kwoze  

Basi wakaondosha lile jiwe. Yesu akainua macho juu, akasema: “Baba, ninakushukuru kwa sababu umenisikia.


Kisha Yesu akatwaa ile mikate mitano na samaki mbili, akainua macho mbinguni, akamushukuru Mungu. Akamega ile mikate, akawapa wanafunzi wake pamoja na zile samaki mbili kusudi waigawanyie watu wote.


Akashika mukono wa mutoto, akamwambia: “Talita kumu,” maana yake: “Kijana binti, ninakuambia, amuka!”


Petro akamwambia: “Ainea, Yesu Kristo anakuponyesha. Simama, ujitandikie kitanda chako wewe mwenyewe.” Na mara moja Ainea akasimama.


Wakati Yesu alipomwona akilia, na wale Wayuda waliokuja pamoja naye wakilia vilevile, akasisimua kwa huzuni nyingi na kufazaika.


Na saa tisa Yesu akalalamika: “Eloi, Eloi, lama sabaktani” maana yake “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”


Yesu akaugua sana kwa huzuni, na kusema: “Sababu gani ninyi watu wa kizazi hiki munataka kuona kitambulisho? Kweli ninawaambia, hamutaonyeshwa kitambulisho!”


Petro akawaamuru watu wote waende inje, akapiga magoti na kuomba. Kisha akaelekea ile maiti na kusema: “Tabita, simama!” Halafu Tabita akafungua macho, na wakati alipomwona Petro akaamuka na kuikaa.


Wakati alipokwisha kusema maneno haya, akaita kwa sauti kubwa, akisema: “Lazaro, toka inje.”


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


Wakati Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akainua macho mbinguni na kusema: “Baba, wakati umetimia. Uonyeshe utukufu wa Mwana wako, kusudi Mwana wako aonyeshe utukufu wako vilevile.


Basi Yesu akasisimua tena kwa huzuni, na kwenda kwenye kaburi. Kaburi lile lilikuwa pango lililofungwa na jiwe kubwa.


Yesu akatoa machozi.


Yesu alipokaribia muji wa Yerusalema, na alipouona, akaulilia,


Yesu akamwambia: “Upate kuona! Imani yako imekuponyesha.”


Kisha akajongea, akagusa sanduku, nao watu waliokuwa wakilibeba wakasimama. Akasema: “Kijana, ninakuamuru, amuka!”


Yesu akamusikilia huruma, akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka utakaswe!”


Alizarauliwa na kukataliwa na watu. Alikuwa mutu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mutu wa kuchukiza kwa watu; alizarauliwa na tukamwona si kitu.


Nyuma ya muda murefu, mufalme wa Misri akakufa. Waisraeli wakaugua na kulia kutokana na hali yao ya utumwa na kilio chao kikamufikia Mungu juu.


Mara moja masikio yake yakafunguka, nao ulimi wake ukafunguliwa, akaanza kusema vizuri.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite