Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 7:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Kisha Yesu akaondoka pale, na kwenda katika jimbo lililokuwa karibu na muji Tiro. Akaingia ndani ya nyumba, naye hakutaka mutu ajue kwamba yuko mule, lakini haikuwezekana kwake kujificha.

Gade chapit la Kopi




Marko 7:24
19 Referans Kwoze  

“Ole kwako, muji Korazini! Ole kwako, muji Betesaida! Kwa maana miujiza iliyofanyika ndani yenu ingalifanyika katika muji wa Tiro na muji wa Sidona, wakaaji wa kule wangekwisha zamani kuvaa magunia na kujipakaa majivu, kwa kuonyesha kwamba wamegeuka toka zambi zao.


Wewe mwanadamu! Umwambie mufalme wa Tiro kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wewe una kiburi cha moyo, na umesema kwamba wewe ni mungu, kwamba umeikalia kiti cha kifalme cha miungu, umekaa mbali huko katika bahari. Lakini, wewe ni mutu tu wala si mungu, ingawa unajiona kuwa na hekima kama mungu.


Na ni hivi vilevile, matendo mazuri yanaonekana waziwazi, na hata yale yasiyoonekana wazi hayawezi kufichwa.


Na wakati Yesu alipoingia ndani ya nyumba, wale vipofu wakamufikia. Naye akawauliza: “Munaamini kwamba ninaweza kuwafanyia jambo hilo?” Nao wakamujibu: “Ndiyo, Bwana.”


Kanana alikuwa babu ya Sidona, muzaliwa wake wa kwanza, na Heti,


Nyuma ya siku chache, Yesu akarudi Kapernaumu, na watu wakasikia kwamba yuko ndani ya nyumba.


Hatalalamika wala hatapiga kelele, wala hatasema kwa sauti kubwa katika barabara.


Alisema: Ewe binti Sidona, hautaweza kufanya sherehe tena; hata ukikimbilia Kipuro, kule nako hautapata pumziko!


“Zebuluni ataishi pembeni ya bahari, kivuko chake kitakuwa pahali pa kuegesha mashua. Mupaka wa inchi yake ni Sidona.


hata eneo la inchi yao likakuwa toka Sidona kuelekea upande wa kusini, kuendelea Gerari mpaka Gaza, na kuelekea upande wa mashariki liliendelea kwa Sodoma na Gomora, Adima na Seboimu mpaka Lasa.


Maovu haya yote yanatoka ndani ya mutu, nayo yanamufanya kuwa muchafu.”


Mwanamuke mumoja, binti yake aliyeshikwa na pepo, akasikia habari za Yesu. Mara moja akamufikia Yesu na kujitupa kwa miguu yake.


Kisha Yesu akaondoka kule katika jimbo lililokuwa karibu na Tiro, akapita Sidona na katikati ya inchi ya Miji Kumi, hata akafika kwenye ziwa la Galilaya.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite