Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Wakawaona wanafunzi wake wamoja wakikula chakula na mikono michafu, maana yake, mikono waliyokosa kunawa kufuatana na desturi ya dini yao.

Gade chapit la Kopi




Marko 7:2
12 Referans Kwoze  

Akawaambia: “Ninyi munajua wazi kama katika Sheria ya dini yetu inakatazwa kwa Muyuda kushirikiana na mutu wa taifa lingine wala kumutembelea. Lakini Mungu amenionyesha kwamba haifai kumuhesabia mutu yeyote kuwa muchafu wala mutengwa.


Kufuatana na vile ninaungana na Bwana Yesu, ninajua hakika kwamba hakuna kitu kinachohesabiwa kichafu katika hali yake ya asili. Lakini kama mutu akihesabu kwamba kitu fulani ni kichafu, basi kitu kile ni kichafu kwake.


Lakini nikajibu: ‘Hapana, hata kidogo, ee Bwana! Ndani ya kinywa changu hamujaingia bado kitu chochote kisichoruhusiwa kukuliwa wala chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu.’


“Kwa sababu gani wanafunzi wako wanavunja desturi za babu zetu kwa kula chakula pasipo kunawa mikono?”


Basi Wafarisayo na walimu wa Sheria wakamwuliza Yesu: “Sababu gani wanafunzi wako hawafuati desturi za babu zetu, lakini wanakula chakula na mikono michafu?”


Mufarisayo yule akashangaa alipoona kwamba Yesu hakunawa mikono mbele ya kula.


Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?


Hakuna kitu chochote kichafu kitakachoingia ndani yake, wala yeye anayefanya machukizo na kusema uongo; lakini wale tu ambao majina yao yaliandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite