49 Nao walipomwona akitembea juu ya maji, wakawaza kwamba ni muzimu, wakaanza kulalamika,
Wakashituka na kuogopa, wakizani kwamba wameona muzimu.
Yeye peke yake alitandaza mbingu, na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.
Aliwaona wanafunzi wake wakitaabika kwa kuendesha chombo sababu upepo ulikuwa ukiwarudisha nyuma. Basi ilipokuwa karibu na mapambazuko, Yesu akawafikia akitembea juu ya maji, akitaka kuwapita.
kwa maana wote walimwona na kuogopa sana. Lakini mara moja Yesu akasema nao na kuwaambia: “Mujipe moyo, ni mimi! Musiogope!”