Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 6:48 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

48 Aliwaona wanafunzi wake wakitaabika kwa kuendesha chombo sababu upepo ulikuwa ukiwarudisha nyuma. Basi ilipokuwa karibu na mapambazuko, Yesu akawafikia akitembea juu ya maji, akitaka kuwapita.

Gade chapit la Kopi




Marko 6:48
16 Referans Kwoze  

Nao walipofika karibu na kile kijiji ambamo walikuwa wakienda, Yesu akaendelea mbele, akiwa sawa mwenye kuwaacha.


Heri watumishi wale atakaowakuta wakikesha hata akifika katikati ya usiku au nyuma ya saa ile.


Yeye peke yake alitandaza mbingu, na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.


Hawakuzaliwa kuwa watoto wa Mungu kwa namna ya kimutu, wala kwa mapenzi ya kimwili, wala kwa mapenzi ya mutu, lakini wamezaliwa na Mungu.


lakini chombo kilikuwa kimekwisha kufika mbali sana na inchi kavu, kikirushwarushwa na zoruba, kwa maana upepo ulikuwa ukitokea mbele.


Ewe Yerusalema, uliteseka, ulitaabishwa na kukosa wa kukufariji, lakini nitakujenga upya kwa mawe ya bei kali, misingi yako itakuwa ya mawe ya yakuti.


umejenga makao yako katika mbingu juu ya maji. Umeyafanya mawingu kuwa gari lako nawe unatembea katika anga.


Yawe ana mamlaka juu mbinguni, ana nguvu kuliko mulio wa bahari, ana nguvu kuliko mawimbi ya maji.


Kesho yake, Saulo aliwagawanya watu katika vikundi vitatu. Wakati wa zamu ya asubui, wakaingia kwenye kambi ya adui, na kuwashambulia Waamoni. Kufikia saa sita za muchana waadui wengi walikuwa wameangamizwa. Wale waliobaki walitawanyika ovyo, hata hakukuwa kikundi chochote kati yao hata cha watu wawili tu pamoja.


Mutu yule alipoona kwamba hawezi kumushinda Yakobo, alimugusa Yakobo kwenye maunganio ya kiuno, naye akateguka alipokuwa anapigana naye.


Akasema: “Bwana zangu, karibu katika nyumba yangu mimi mutumishi wenu. Munaweza kunawa miguu na kulala kwangu usiku wa leo. Asubui mapema mutaweza kuendelea na safari yenu.” Lakini, wao wakasema: “Hapana! Sisi tutalala huku katika barabara.”


Karibu na mapambazuko, Yawe akaangalia jeshi la Wamisri kutoka katika ule munara wa moto na ule munara wa wingu, akalitia hofu kubwa.


Munajua vema kwamba mwenye nyumba angalijua wakati gani mwizi atakapokuja kuiba, angalikesha na kuchunga nyumba yake isibomolewe.


Giza lilipoingia, chombo kilikuwa katikati ya ziwa, na Yesu alikuwa peke yake inchi kavu.


Nao walipomwona akitembea juu ya maji, wakawaza kwamba ni muzimu, wakaanza kulalamika,


Basi muangalie sababu hamujui wakati bwana wa nyumba atakaporudi: labda magaribi, au katikati ya usiku, au wakati jogoo anapowika, au asubui.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite