36 Uwaage watu hawa kusudi waende kwenye nyumba kule katika mbuga na katika vijiji vya hapa karibu wapate kujinunulia chakula.”
Lakini Yesu hakumujibu hata neno moja. Halafu wanafunzi wake wakamufikia na kumusihi: “Umwambie aende kwa maana anatuuzi na makelele.”
Wanafunzi wake wakamujibu: “Hauoni namna watu wanavyokusongasonga? Namna gani unauliza kwamba ni nani aliyekugusa?”
Wandugu zake za jamaa waliposikia maneno haya, wakaondoka kwenda kumutwaa, kwa maana walisema kwamba amepotelewa na akili.
Basi Petro akamwita Yesu pembeni na kuanza kumukaripia, akisema: “Ee Bwana, isikuwe vile! Mambo yale hayatakufikia hata kidogo!”
Ilipofika saa za magaribi, wanafunzi wa Yesu wakamufikia na kumwambia: “Hapa ni pori na sasa ni magaribi.
Yesu akawajibu: “Ninyi wenyewe muwape chakula.” Lakini wakamwuliza: “Unataka tuende kununua mikate kwa bei ya vikoroti mia mbili vya feza?”