Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 6:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Wakati Yesu alipotoka ndani ya chombo, akaona kundi kubwa la watu, akawasikilia huruma, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasiokuwa na muchungaji. Basi akaanza kuwafundisha maneno mengi.

Gade chapit la Kopi




Marko 6:34
19 Referans Kwoze  

Yesu alipoona kundi la watu, aliwasikilia huruma, kwa maana walikuwa wamesumbuka na kuregea, kama kondoo wasiokuwa na muchungaji.


ambaye atawatangulia na kuwaongoza katika shuguli zao zote, kusudi wasikuwe kama kondoo wasiokuwa na muchungaji.


Lakini makundi ya watu walipopata habari ile, wakamufuata mpaka kule. Yesu akawapokea na kuanza kusema nao juu ya Ufalme wa Mungu, na vilevile akawaponyesha wale waliohitaji kuponyeshwa.


Sanamu zao za kupigia ramuli ni uongo mutupu, na waaguzi wao wanaagua uongo; watabiri wao wanatabiri ndoto danganyifu, na kuwapa watu faraja za bure. Ndiyo maana watu wa Yuda wanatangatanga kama kondoo; wanataabika maana wamekosa muchungaji.


Watu wangu walikuwa kama kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha, wakawageuza kuelekea kwenye milima; walitembea toka mulima mpaka kilima, wakasahau makao yao.


Naye Mikaya akasema: “Niliwaona watu wote wa Israeli wakitawanyika juu ya milima kama kondoo wasiokuwa na muchungaji. Naye Yawe akasema: ‘Watu hawa hawana kiongozi; uwaache warudi kila mutu kwake kwa amani.’ ”


Halafu, Mikaya akasema: “Niliona watu wote wa Israeli wametawanyika juu ya milima kama kondoo wasiokuwa na muchungaji. Naye Yawe akasema: ‘Watu hawa hawana kiongozi. Basi warudi kila mutu kwake kwa amani.’ ”


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


Yesu alipotoka ndani ya chombo, akaona kundi kubwa la watu, naye akawasikilia huruma, akawaponyesha wale waliokuwa wagonjwa kati yao.


Kwa hiyo ilimupasa afanane na wandugu zake katika mambo yote, kusudi apate kuwa Kuhani Mukubwa anayekuwa mwenye huruma na mwaminifu katika kazi yake mbele ya Mungu, na kwa njia hiyo zambi za watu zisamehewe.


Yesu akawaita wanafunzi wake, na kuwaambia: “Ninawasikilia watu hawa huruma, kwa sababu wamekaa nami sasa kwa muda wa siku tatu, nao hawana chakula tena. Nami sitaki kuagana nao pasipo kula, kusudi wasiregee katika njia.”


Kama swala anayewindwa, kama kondoo wasiokuwa na muchungaji, kila mumoja atajiunga na watu wake, kila mutu atakimbilia katika inchi yake.


Basi, kwa sababu hao kondoo hawakuwa na muchungaji, walisambazwa na kuwa chakula cha nyama wa pori.


Lakini watu wengi waliwaona wakiondoka, wakawatambua. Kwa hiyo wakaenda kule mbio kwa miguu toka miji yote, wakawatangulia kule walipokuwa wakienda.


Ilipofika saa za magaribi, wanafunzi wa Yesu wakamufikia na kumwambia: “Hapa ni pori na sasa ni magaribi.


Katika siku zile kundi kubwa la watu walikusanyika tena. Nao walipokosa chakula, Yesu akawaita wanafunzi wake, na kuwaambia:


“Ninawasikilia watu hawa huruma, kwa sababu wamekaa nami sasa muda wa siku tatu, nao hawana chakula tena.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite