Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 6:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Lakini wengine walisema: “Huyu ni nabii Elia.” Wengine walisema: “Yeye ni nabii sawa na mumoja wa wale manabii wa zamani.”

Gade chapit la Kopi




Marko 6:15
19 Referans Kwoze  

Kundi la watu wakajibu: “Huyu ni nabii Yesu wa Nazareti katika Galilaya.”


Nao wakamujibu: “Wamoja wanasema kwamba wewe ni Yoane Mubatizaji; wengine wanasema kwamba wewe ni nabii Elia na wengine wanasema kwamba wewe ni mumoja wa manabii wengine.”


Nao wakamujibu: “Wamoja wanasema kwamba yeye ni Yoane Mubatizaji; wengine wanasema kwamba yeye ni Elia, na wengine wanasema ni Yeremia au mumoja wa manabii wengine.”


Wafarisayo wakamwuliza tena yule aliyekuwa kipofu: “Na wewe unasema nini juu ya yule aliyekuponyesha macho?” Akajibu: “Yeye ni nabii.”


Watu wamoja katika kundi lile waliposikia maneno hayo, wakasema: “Hakika mutu huyu ndiye Nabii aliyepaswa kuja!”


Watu walipoona kile kitambulisho Yesu alichoonyesha, wakasema: “Hakika mutu huyu ndiye yule nabii aliyepaswa kuja katika dunia!”


Wakamwuliza Yoane: “Ikiwa wewe si Kristo, wala Elia, wala yule nabii, basi sababu gani unabatiza?”


Halafu wakamwuliza: “Basi wewe ni nani? Wewe ni Elia?” Yoane akajibu: “Mimi si yeye.” Wakamwuliza tena: “Wewe ni yule nabii?” Naye akawajibu: “Hapana.”


Nao wakajibu: “Wamoja wanasema kwamba wewe ni Yoane Mubatizaji, wengine wanasema kwamba wewe ni Elia, na wengine wanasema kwamba wewe ni mumoja wa manabii wa zamani aliyefufuka.”


Na wengine walikuwa wakisema kwamba Elia ametokea. Na wengine walisema kwamba mumoja wa manabii wa zamani amefufuka.


Yule Mufarisayo aliyemwalika Yesu alipoona vile, akajisemesha: “Kama mutu huyu angekuwa kweli nabii, angetambua mwanamuke huyu anayemugusa ni wa namna gani. Angetambua kwamba yeye ni mwenye mwenendo mubaya.”


Watu wote wakashikwa na woga, nao wakamutukuza Mungu, wakisema: “Nabii mukubwa ametokea tena kwetu! Mungu amekuja kuwasaidia watu wake.”


Atatangulia mbele ya kufika kwa Bwana, akiwa na roho na uwezo kama nabii Elia, kwa kuwapatanisha tena baba na watoto wao, na kuwageuza waasi wapate kuwa na hekima kama vile wenye haki. Hivi atamutayarishia Bwana watu wanaokuwa tayari kwa kumupokea.”


Lakini Herode aliposikia habari zile, akasema: “Ni yule Yoane Mubatizaji niliyemukata kichwa ndiye amefufuka!”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite