Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 6:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Mufalme Herode alisikia habari za Yesu, kwa maana jina lake lilikuwa limevuma fasi zote. Watu wamoja walisema: “Huyu ni Yoane Mubatizaji aliyefufuka! Ni kwa sababu hii amepata uwezo wa kufanya miujiza.”

Gade chapit la Kopi




Marko 6:14
16 Referans Kwoze  

Kwa maana tokea kwenu neno la Bwana lilienea, si katika Makedonia na Akaya tu, lakini habari za imani kwa Mungu zilisambaa fasi zote, hata sisi hatukukuwa tena na lazima ya kusema neno juu ya ile.


Kwa saa zile Wafarisayo wamoja walimwendea Yesu na kumwambia: “Ondoka hapa uende fasi ingine, maana mufalme Herode anataka kukuua.”


Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Tiberio mufalme wa Roma, Pontio Pilato alikuwa liwali wa jimbo la Yudea, na Herode alikuwa mutawala wa jimbo la Galilaya na ndugu yake Filipo alikuwa mutawala wa inchi ya Iturea na ya Tarakoniti. Vilevile Lisania alikuwa mutawala wa inchi ya Abilene,


Nao wakamujibu: “Wamoja wanasema kwamba wewe ni Yoane Mubatizaji; wengine wanasema kwamba wewe ni nabii Elia na wengine wanasema kwamba wewe ni mumoja wa manabii wengine.”


Lakini mutu yule alipoenda, akaanza kutangaza habari zile fasi zote. Na kwa sababu hii Yesu hakuweza kuingia tena waziwazi katika muji wowote, lakini alibaki mbali nayo pahali penye ukiwa. Na watu walimufikia kule kutoka pande zote.


Halafu sifa za Yesu zikaenea upesi katika jimbo lote la Galilaya.


Lakini wakaenda na kuanza kutangaza habari za Yesu katika inchi ile yote.


Kule Yerusalema wafundi wake wakamutengenezea mitambo ya kurushia mishale na mawe makubwamakubwa. Sifa zake zikaenea kila pahali, nguvu zake zikaongezeka zaidi kwa sababu ya usaidizi mwingi alioupata kutoka kwa Mungu.


Waamoni walimulipa kodi, na sifa zake zikaenea mpaka Misri, kwa sababu alipata nguvu.


Nao wakajibu: “Wamoja wanasema kwamba wewe ni Yoane Mubatizaji, wengine wanasema kwamba wewe ni Elia, na wengine wanasema kwamba wewe ni mumoja wa manabii wa zamani aliyefufuka.”


Mungu vilevile alihakikisha ushuhuda wao kwa njia ya maajabu, ya miujiza mbalimbali, na ya vitambulisho, na kwa njia ya zawadi za Roho Mutakatifu alizowapa watu kama anavyopenda.


Na jambo hili Yesu alilolifanya likaenea katika Yudea yote na katika inchi zote zinazokuwa pembeni.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite