13 Wakafukuza pepo wengi, na wakapakaa wagonjwa wengi mafuta na kuwaponyesha.
Wale wanafunzi makumi saba wakarudia wakijazwa na furaha, nao wakasema: “Bwana, hata pepo wanatutii tunapowaamuru kwa jina lako!”
Aliwaita wanafunzi wake kumi na wawili, akaanza kuwatuma wawili wawili na kuwapatia uwezo wa kufukuza pepo.
Habari zake zikavuma katika inchi yote ya Suria. Wakamuletea watu wote walioteswa na magonjwa mbalimbali na wenye maumivu ya kila namna, wenye pepo, wenye kifafa na wenye kupooza, naye Yesu akawaponyesha.