42 Mara moja yule kijana akasimama na kuanza kutembea (alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili). Nao watu wakashangaa sana kwa kuona jambo hilo.
Nao watu wakashangaa sana na kusema: “Mambo anayofanya ni mazuri kweli. Anawawezesha hata viziwi wasikie, nao wabubu wapate kusema.”
Kisha akaingia ndani ya chombo walimokuwa, na upepo ukakoma. Kwa hiyo wanafunzi wakashangaa sana,
Halafu wakaogopa sana, nao wakaanza kuulizana: “Huyu ni mutu gani, hata zoruba na ziwa vinamutii?”
Watu wote wakashangaa sana na kuulizana: “Hatujaona mambo kama haya! Hakika mafundisho haya ni yenye mamlaka! Mutu huyu anaamuru hata pepo, nao wanamutii!”
Akashika mukono wa mutoto, akamwambia: “Talita kumu,” maana yake: “Kijana binti, ninakuambia, amuka!”
Lakini Yesu aliwaagiza sana wasimwambie mutu yeyote jambo lililofanyika. Kisha akawaambia wamupe mutoto yule chakula.