Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 5:36 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

36 Lakini Yesu hakuangalia maneno yao, akamwambia yule mukubwa: “Usiogope, uamini tu.”

Gade chapit la Kopi




Marko 5:36
11 Referans Kwoze  

Lakini Yesu aliposikia vile, akamwambia Yairo: “Usiogope, amini tu, atapona.”


Yesu akamwambia: “Sikukuambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?”


Yesu akamwambia: “Kwa sababu gani unasema: ‘Kama unaweza?’ Yote yanawezekana kwa yule anayeamini.”


Yesu akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponyesha. Ujiendee na amani, ugonjwa wako umepona!”


Yesu akawajibu: “Kwa sababu imani yenu ni ndogo. Kweli ninawaambia kama mukiwa na imani, hata ikiwa tu kama punje ndogo sana ya mbegu ya haradali, mutaweza kuuambia mulima huu: ‘Toka hapa uende kule,’ nao utatoka pale. Hakuna kitu chochote kitakachokosa kuwezekana kwenu. [


Kesho yake, wakaamuka asubui mapema, wakaenda mpaka katika jangwa la Tekoa. Walipokuwa wanaondoka, Yosafati akasimama, akawaambia: “Musikilize, enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema! Mumwamini Yawe, Mungu wenu, nanyi mutakuwa imara. Muwaaminie manabii wake, nanyi mutashinda.”


Yesu alipokuwa hajamaliza kusema maneno hayo, mukubwa mumoja akafika, akapiga magoti mbele yake na kumwambia: “Binti yangu anakufa sasa hivi; lakini kuja, uweke mikono yako juu yake kusudi apate kufufuka.”


Halafu mukubwa mumoja wa nyumba ya kuabudia aliyeitwa Yairo, akafika pale. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele yake,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite