Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 5:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 akamusihi sana, akisema: “Binti yangu mudogo yuko karibu kufa. Ninakuomba ukuje kwanza kwa kuweka mikono yako juu yake, kusudi apate kupona na kuishi!”

Gade chapit la Kopi




Marko 5:23
26 Referans Kwoze  

Halafu akaweka mikono juu yake kwa kumuponyesha. Na mara moja akainuka tena, na kumutukuza Mungu.


Jua lilipotua, wakamuletea Yesu watu wote wenye kuwa na magonjwa mbalimbali. Akaweka mikono yake juu ya kila mumoja wao, akawaponyesha.


wakishika nyoka au kunywa sumu yoyote, hawatakufa. Wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapona.”


Baba ya Publio alikuwa amelala kwa ajili ya kuwezwa na ugonjwa wa homa na wa kuhara damu. Paulo akaenda kumwangalia, akamwombea na kuweka mikono juu yake, naye akapona.


Yesu akatoka ndani ya ile nyumba ya kuabudia, akaenda kwa nyumba ya Simoni. Mama mukwe wa Simoni alikuwa ameshikwa na homa kali, halafu wakamwomba Yesu amuponyeshe.


Yesu akashika mukono wa yule kipofu na kumupeleka inje ya kijiji. Yesu alipokwisha kupakaa mate kwa macho ya mutu yule na kuweka mikono juu yake, akamwuliza: “Unaona kitu?”


Wakamuletea mutu mumoja aliyekuwa kiziwi na mwenye kigugumizi vilevile. Wale waliomuleta wakamusihi Yesu amuponyeshe kwa kuweka mikono juu yake.


Alipokaribia kwenye mulango wa ukuta wa muji, kukatokea watu wanaobeba maiti ya kijana mumoja aliyekuwa mutoto wa pekee wa mama mumoja mujane. Nao watu wengi wa muji ule walikuwa wakimusindikiza yule mama.


Wakafukuza pepo wengi, na wakapakaa wagonjwa wengi mafuta na kuwaponyesha.


Yesu akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka, utakaswe!” Na mara moja mutu yule akatakaswa ukoma wake.


Halafu katika taabu yao wakamulilia Yawe, naye akawaokoa katika mateso yao.


Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Lakini Namani alikasirika sana, akaenda zake akisema: “Nilizani kwamba hakika atanifikia na kumwomba Yawe, Mungu wake, apitishe mikono yake juu ya pahali ninapogonjwa na kuniponyesha!


Basi Anania akaenda. Alipofika ndani ya nyumba ambamo Saulo alikuwa, akaweka mikono juu yake na kumwambia: “Ndugu Saulo, Bwana Yesu aliyekutokea katika njia ulipokuwa ukikuja huku, amenituma kusudi upate kuona tena na kujazwa na Roho Mutakatifu.”


Kisha wakawaweka mbele ya mitume, nao wakaomba na kuweka mikono juu yao.


Hawa wadada wawili wakatuma habari hii kwa Yesu: “Bwana, rafiki yako mupendwa ni mugonjwa.”


Basi Yesu akaenda pamoja naye. Watu wengi walimufuata na kumusongasonga.


Halafu Petro na Yoane wakaweka mikono juu yao, nao wakapokea Roho Mutakatifu.


Yeye ameona katika maono mutu mumoja anayeitwa Anania, akiingia ndani ya nyumba na kuweka mikono juu yake kusudi apate kuona tena.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite