19 Yesu hakumuruhusu, lakini akamwambia: “Kwenda kwako kwenye jamaa yako, na uwaelezee mambo Bwana aliyokutendea na namna alivyokuhurumia.”
Enyi munaomwabudu Mungu, mukuje wote musikilize, nami nitawaelezea mambo aliyonitendea.
“Mukuje mumwone mutu aliyeniambia maneno yote niliyotenda. Huyu si Kristo?”
“Rudia kwako na ueleze mambo yote Mungu aliyokutendea.” Basi yule mutu akajiendea, na kutangaza fasi zote katika muji wake mambo Yesu aliyomutendea.
Basi yule mutu akajiendea, akaanza kutangaza mambo yote Yesu aliyomutendea katika inchi ya Miji Kumi. Na watu wote waliomusikia wakashangaa sana.
Namani alipopata habari hii, akaenda kwa mufalme na kumwelezea habari za mutoto yule.