Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 4:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Lakini mbegu zingine zikaanguka katika udongo muzuri, mimea ikaota, ikakomaa na kuzaa matunda: zimoja zikazaa punje makumi tatu, zingine makumi sita na zingine punje mia moja.”

Gade chapit la Kopi




Marko 4:8
21 Referans Kwoze  

“Mimi ni muzabibu, nanyi ni matawi. Anayekaa ndani yangu, na mimi ndani yake anazaa matunda mengi, kwa sababu pasipo mimi hamuwezi kufanya kitu.


Habari Njema ile inatoa matunda na kuenea katika dunia yote sawa vile ilivyofanya kwenu tangu siku ile muliposikia wakisema juu ya neema ya Mungu na kupata kuitambua inavyokuwa kweli.


Nao udongo muzuri, walimopanda mbegu, ni mufano wa watu wanaosikia Neno la Mungu na kulipokea. Nao wanazaa matunda; wamoja matunda makumi tatu, wengine makumi sita na wengine mia moja.”


Mwaka ule Isaka akapanda mbegu katika inchi ile, akavuna mara mia zaidi, maana Yawe alimubariki,


Watu hao walikuwa wenye nia nzuri zaidi kuliko watu wa Tesalonika; nao walipokea Neno la Mungu kwa hamu kubwa. Kila siku walichunguza Maandiko Matakatifu wapate kujua kwamba maneno Paulo aliyosema yalikuwa ya haki.


Lakini mbegu zingine zikaanguka katika udongo muzuri na kutoa matunda: zimoja zikazaa punje mia moja, zingine makumi sita na zingine makumi tatu.


Neno langu ni kama moto. –Ni ujumbe wa Yawe!– Neno langu ni kama nyundo inayovunja mawe vipandevipande.


Maisha yenu yatajazwa matendo ya haki ambayo Yesu Kristo anayowajalia, kwa ajili ya utukufu na sifa ya Mungu.


Kama mutu akitaka kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu, au kama ninasema kwa mamlaka yangu mwenyewe.


Nao udongo muzuri walimopanda mbegu, ni mufano wa watu wanaosikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mwema na kwa uhaki. Ndio wale wanaovumulia hata wanatoa matunda mazuri.


Lakini mbegu zingine zikaanguka katika udongo muzuri; nazo zikaota na kutoa matunda, kila moja punje mia.” Yesu alipokwisha kuwaambia hayo yote, akasema: “Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!”


Pahali zile mbegu zilipoanguka katika udongo muzuri ni mufano wa watu wanaosikia Neno la Mungu na kulielewa. Nao wanazaa matunda; wamoja matunda mia moja, wengine makumi sita na wengine makumi tatu.”


Yawe anasema: Piga kelele, wala usijizuize; ulalamike kwa sauti kubwa kama baragumu. Uwatangazie watu wangu makosa yao, uwaambie wazao wa Yakobo zambi zao.


Mbegu zingine zilianguka katikati ya miiba. Ile miiba ikaota na kuzisonga mbegu hata hazikuweza kutoa kitu.


Kisha akawaambia: “Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!”


Katika kuungana naye, jengo lote nzima linaunganishwa vizuri na kuongezeka hata lipate kuwa hekalu takatifu kwa ajili ya Bwana.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite