Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 4:39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

39 Yesu akaamuka, akakaripia ile zoruba na kuiambia ziwa: “Kimya! Tulizana!” Basi zoruba ikakoma na kukakuwa kimya kabisa.

Gade chapit la Kopi




Marko 4:39
21 Referans Kwoze  

Alituliza ile zoruba kali, nayo mawimbi yakanyamaza.


Ee Yawe, Mungu wa majeshi, ni nani mwenye nguvu kama wewe? Ee Yawe, uaminifu umekuzunguka pande zote.


Kwa nguvu yako uliisimika milima pahali pake. Wewe una nguvu nyingi!


Yawe ameikaa juu ya mafuriko ya maji; Yawe ni mufalme anayetawala milele.


Mbona hamuniogopi? –Ni ujumbe wa Yawe.– Kwa nini hamutetemeki mbele yangu? Mimi niliwekea bahari muchanga kuwa mupaka wake; ni kizuizo cha milele ambacho bahari haiwezi kuvuka. Ingawa mawimbi yanaupiga, hayawezi kuupita; ingawa yanavuma, hayawezi kuuruka.


wakati alipowekea bahari mupaka wake kusudi maji yake yasipate kuvunja amri yake, wakati alipoweka misingi ya dunia.


Mumusifu, enyi moto, mvua ya mawe na teluji, upepo wenye zoruba unaotimiza amri yake!


na kuiambia: “Mwisho wako ni hapa, si zaidi! Mawimbi yako ya nguvu yatakomea hapa!”


Waisraeli wakapita katikati ya bahari pahali pakavu, kuta za maji zikiwa upande wao wa kuume na wa kushoto.


Wakati Yesu alipoona watu wengi wanazidi kukusanyika mbiombio, akamukaripia yule pepo na kumwambia: “Wewe pepo wa bubu na wa kiziwi, ninakuamuru utoke ndani ya mutu huyu wala usimurudilie tena!”


Inua fimbo yako na kuielekeza juu ya bahari. Maji yatagawanyika na Waisraeli wataweza kuvuka katikati ya bahari pahali pakavu.


Basi akainama kunapokuwa yule mama, akaamuru ile homa itoke ndani yake, naye akapona. Na mara moja akasimama na kuanza kuwashugulikia.


Anaikaripia bahari na kuikausha, yeye anaikausha mito yote. Mbuga za Basani na mulima Karmeli zinanyauka, maua ya Lebanoni yanakauka.


Yawe hatatutupilia milele.


Yesu akawajibu: “Sababu gani munaogopa kama hivi? Hakika imani yenu ni ndogo!” Halafu akasimama, akakaripia zoruba na maji na kukakuwa kimya kabisa ndani ya ziwa.


Yesu alikuwa upande wa nyuma wa chombo, akilala usingizi akilalisha kichwa juu ya mufuko wa kuegemea. Wanafunzi wake wakamwamusha na kumwambia: “Mwalimu, haikuhangaishi kuona sisi tunakufa?”


Yesu akamukaripia, akimwamuru hivi: “Nyamaza, na utoke ndani ya mutu huyu!” Na yule pepo akamutupa yule mutu chini mbele ya watu, na kutoka ndani yake pasipo kumwumiza.


Basi wanafunzi wake wakamujongelea, wakamwamusha wakisema: “Bwana, Bwana, tunakufa!” Yesu alipoamuka, akakaripia zoruba, nayo ikakoma na maji yakatulia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite