Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 4:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

35 Na ilipotimia magaribi siku ile ile, Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Tuvuke ngambo ingine ya ziwa.”

Gade chapit la Kopi




Marko 4:35
11 Referans Kwoze  

Yesu alipoona kundi la watu wakimuzunguka, akatoa amri ya kuvuka ngambo ingine ya ziwa.


Halafu akawaambia wanafunzi wake: “Imani yenu iko wapi?” Nao wakaogopa na kushangaa, wakiulizana: “Huyu ni mutu gani? Anaamuru hata zoruba na ziwa, navyo vinamutii!”


Siku moja Yesu akaingia ndani ya chombo pamoja na wanafunzi wake. Naye akawaambia: “Tuvuke ngambo ya ziwa.” Basi wakaondoka.


Mara moja kisha mambo hayo, Yesu akawalazimisha wanafunzi wake waingie ndani ya chombo na kumutangulia ngambo ingine ya ziwa. Kwa wakati ule yeye alibaki akiaga lile kundi la watu.


Kisha akawaacha, akaingia tena ndani ya chombo, akaanza kuvuka ziwa.


Watu wale wakamukuta Yesu kule ngambo ya ziwa na kumwuliza: “Mwalimu, ulifika hapa wakati gani?”


Wakaingia ndani ya chombo, wakaanza kuvuka ziwa kwa kwenda Kapernaumu. Giza lilikuwa limekwisha kuwa, na Yesu alikuwa hajarudi kukutanana nao.


Nyuma ya maneno hayo, Yesu akavuka ziwa la Galilaya (linaloitwa vilevile Tiberia).


Pale pale Yesu akawalazimisha wanafunzi wake waingie ndani ya chombo na kumutangulia ngambo ingine ya ziwa la Galilaya kuelekea muji Betesaida. Kwa wakati ule alibaki akiaga lile kundi la watu.


Yesu akavuka ngambo ingine ya ziwa la Galilaya. Alipokuwa pembeni ya ziwa, watu wengi wakakusanyika karibu naye.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite