35 Kwa sababu mutu yeyote anayefanya mapenzi ya Mungu, huyu ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu.”
Dunia inapita pamoja na tamaa zake, lakini mutu yule anayefanya mapenzi ya Mungu anaishi milele.
“Si kila mutu anayeniita ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni, lakini yule tu anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.
Kama mutu akitaka kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu, au kama ninasema kwa mamlaka yangu mwenyewe.
Lakini mutu anayechunguza sheria kamilifu inayoweka watu huru na kuendelea kushikamana nayo, na si kuisikia tu na kisha kuisahau, lakini anaitimiza kabisa, mutu huyu atabarikiwa na Mungu katika shuguli zake.
Musitumike tu wakati wanapowaangalia, mukitafuta kuwapendeza. Lakini mutimize mapenzi ya Mungu kwa moyo wote mukijihesabu kama watumwa wa Kristo.
Munapaswa kuvumilia, kusudi mutimize mapenzi ya Mungu, na kuweza hivi kupewa kile mulichoahidiwa.
Sasa, musiishi tena kufuatana na tamaa za kimutu, lakini muishi kufuatana na mapenzi ya Mungu kwa muda unaowabakilia kwa kukaa katika dunia.